Page 144 - Fasihi_Kisw_F5
P. 144

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 5.10
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandao,  maktaba  au matukio  halisi,  kusanya
              mazungumzo  ya  makundi  mawili  (mtoto  au  watoto  wadogo wenye  umri  wa
              kuanza shule na kiongozi yeyote wa serikali kisha tathmini  aina, maana na
          FOR ONLINE READING ONLY
              mpangilio wa hoja zinazotolewa katika mazungumzo ya kila kundi.


              Misingi ya ujenzi wa hoja zenye mantiki na ushawishi
              Ujenzi wa hoja zenye mantiki na ushawishi humtaka mtoahoja awe razini na
              makini.  Hoja hizo hujengwa kwa kuzingatia  misingi ya uadilifu,  ushawishi,
              kudhihirisha uhakika wa jambo, hadhira, muundo, na mpangilio wa kimantiki.


              Kwa muktadha wa ujenzi wa hoja, dhana ya uadilifu hujumuisha hali za ukweli,
              usawa, heshima, usahihi, na uhalisi  wa jambo  linalowasilishwa. Mjengahoja
              hutakiwa kuepuka kuwasilisha jambo kwa namna ya kumshambulia au kumbeza
              mtu. Pia, hutakiwa kuwasilisha jambo lenye ukweli na la usahihi. Atumie data
              sahihi ili kuipa nguvu hoja yake. Hivyo, hadhira yake itavutiwa na kuamini hoja
              zake.

              Mjengahoja pia hutakiwa kuwasilisha hoja zake kwa ufasaha. Aoneshe kujiamini
              ili  aiaminishe hadhira  yake  kuwa ana  uhakika  na anachokiwasilisha.  Katika
              maelezo  ya hoja yake, aoneshe ufundi wa kuhusisha mifano  na mazingira
              halisi. Kwa kufanya hivi, huonesha mamlaka  ya kimaarifa  na kiujuzi juu ya
              anachokiwasilisha; na hadhira hupata imani kuwa inapokea hoja kutoka kwa mtu
              sahihi.

              Pia, mjengahoja hutakiwa kutumia mbinu ya ushawishi kwa hadhira yake juu
              ya kinachowasilishwa. Mjenzi mzuri wa hoja huzingatia suala la kugusa hisi za
              hadhira yake ili kuihamasisha kupokea, kuamini na kutumia hoja zake. Nguvu ya
              ushawishi husaidia kuimarisha kile kilichomo katika akili ya hadhira. Pia, kama
              hadhira ilikuwa katika  uelekeo tofauti  wa jambo  linalowasilishwa, ushawishi
              husaidia kuivutia kwenye uelekeo wa mwasilishaji. Mbinu za kujenga ushawishi
              ni pamoja na kutumia mifano halisi, mbazi, simulizi fupi, uteuzi wa maneno
              yenye  uwezo  wa kuamsha  hisia  za  hadhira,  na  semi  mbalimbali  kama  vile
              misemo, methali, nahau na misimu.


              Kadhalika,  mjengahoja  anapaswa kuzingatia  hali ya hadhira. Hali ya hadhira
              hujumuisha uwezo wa kuelewa, wastani wa kiwango cha elimu, wastani wa
              tajiriba  ya maisha, mwelekeo  wa malengo,  matarajio,  utamaduni,  pamoja  na
              hali ya kisaikolojia. Uzingatizi wa hali hizo za hadhira humsaidia mjenga hoja



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           133
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   133                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   133
   139   140   141   142   143   144   145   146   147   148   149