Page 145 - Fasihi_Kisw_F5
P. 145

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari



              kuteua na kutumia maneno, vipamba-lugha (kama vile toni na kidatu), na mifano
              muafaka.  Vilevile,  humsaidia  kutathimini  uelewekaji  wa  wasilisho  wakati
              anaendelea kujenga hoja.


              Isitoshe, mjengahoja anapaswa kuzingatia  muundo mzuri. Mjenzi mzuri wa
          FOR ONLINE READING ONLY
              hoja lazima atafakari suala hili ambalo lina athari kubwa katika mpangilio wa
              anachowasilisha. Hata kama hoja yake ni moja, lazima aiunde vyema. Ajiulize
              kuhusu nini kianze kuwasilishwa na nini kifuatie. Kama hoja zipo zaidi ya moja,
              atafakari  kuhusu kubebana, kusababishana na kuendelezana  kwa hoja hizo.
              Hivyo, ni vyema aliunde wasilisho lake katika namna inayorahisisha kueleweka
              kwake.


              Kutathmini kazi za fasihi kwa  kutumia  misingi ya ujenzi wa hoja
              zenye mantiki na ushawishi
              Misingi ya ujenzi wa hoja zenye mantiki na ushawishi hutumiwa pia kutathmini
              vipengele mbalimbali vya fani na maudhui katika kazi za fasihi. Misingi ambayo
              hutumika  kujenga  hoja  zenye  mantiki  na  ushawishi  ni  pamoja  na  uadilifu,
              ushawishi, kudhihirisha  mamlaka,  na  kutilia  maanani  hadhira  na  muundo.
              Miongoni  mwa  vipengele vilivyomo  katika  kazi  ya  fasihi  ambavyo  huweza
              kutathminiwa ni matendo ya wahusika ambayo yakisawiriwa vyema hudhihirisha
              hoja zenye mantiki.

               Shughuli ya 5.11

              (a)  Kwa kutumia kipande kifuatacho cha tamthiliya, jenga hoja zenye mantiki
                   na ushawishi kuhusu ujenzi wa wahusika.

                   Mlinzi I:        We, we … simama! (Anamkaribia Mwari I)

                                    Nasema simama … nani aliyekutieni msuko huu?

                                      Nani kakutieni damu mpya? Mlikuwa watulivu nyinyi …
                                    We… wewe… (Mlinzi anamfikia na kumkamata mkono
                                    mwari)

                   Mwari I:           Nyeupe ni nyeupe na nyeusi ni nyeusi … na nyekundu ni
                                    nyekundu, nyekundu haiwezi kuwa manjano …


                   Mlinzi I:          Sharrab! Unajuaje wewe? Nyeupe ni nyeusi na nyeusi ni
                                    nyeupe na nyekundu kila siku ni manjano …





               134                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   134                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   134
   140   141   142   143   144   145   146   147   148   149   150