Page 150 - Fasihi_Kisw_F5
P. 150

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Mwenyekiti wa Jopo:      Bi. Nagona, jopo limekusikiliza na kukagua vyeti
                                           vyako.  Tunakuruhusu uende.  Nasi tunaendelea
                                           kukamilisha    mchakato     huu.   Tutakujulisha
                                           matokeo yoyote yatakayoamuliwa  kwa kutumia
          FOR ONLINE READING ONLY
                                           mawasiliano uliyoyaweka katika barua ya maombi
                                           pamoja na taarifa za wasifu kazi wako.

                   Nagona:                  Asanteni sana, ninasubiri  kwa hamu  matokeo
                                           hayo. Je, ni lini yanatarajiwa kuwa tayari?


                   Mwenyekiti wa Jopo:     Ndani ya juma moja kuanzia leo utapata majibu.

                   Nagona:                 Asanteni, na kwa kwaherini.

                   Maswali


                   (i)  Kwa nini unafikiri utambulisho ni muhimu katika usaili?
                   (ii)  Je, unafikiri hoja za msailiwa zilikuwa na mantiki na ushawishi? Kwa
                        nini?

                   (iii)  Ni maeneo yapi msailiwa ametumia maarifa ya kifasihi kujenga hoja
                        zake?

                   (iv)  Ungekuwa Nagona, ungejibuje swali kutoka kwa Mjumbe wa 1,
                        Mjumbe wa 3 na Mjumbe wa 4?

              (b)  Tumia  maarifa  ya  kifasihi kuwasilisha  hoja  zenye  mantiki  na  ushawishi
                   wakati wa kuigiza kama msailiwa wa nafasi ya kazi.

              (c)  Tumia  maarifa  ya  kifasihi kuwasilisha  hoja  zenye  mantiki  na  ushawishi

                   wakati wa kuigiza kama mgombea wa nafasi ya uongozi katika uchaguzi
                   wa shuleni kwenu.
               Shughuli ya 5.13

              Chagua mada mojawapo kati ya zifuatazo, kisha andaa hoja unazoweza kuwasilisha
              katika malumbano ya hoja kwa kutumia maarifa ya kifasihi kuwasilisha hoja
              zenye mantiki na ushawishi.

              (i)  Athari za utandawazi kwa vijana

              (ii)  Mchango wa fasihi katika utunzaji wa mazingira




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           139
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   139                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   139
   145   146   147   148   149   150   151   152   153   154   155