Page 154 - Fasihi_Kisw_F5
P. 154

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              hujumuisha matini iliyo katika umbo la utungo mmoja kama vile semi mbalimbali,
              hadi matini zenye mchanganyiko wa mambo mengi. Mifano ya matini hizo ni
              insha za kifasihi, ushairi, tamthiliya, hadithi fupi, na riwaya. Kazi changamani
              ni zile zenye mchanganyiko wa mbinu nyingi za kisanaa. Pia, kazi hizi huwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              na idadi kubwa ya vipengele kama vile vya wahusika, visa, mikasa, migogoro,
              mandhari na dhamira.

              Kubuni ni mchakato wa kusawiri mawazo kwa kutumia mbinu za kisanaa.
              Mchakato huu huweza kufanyika katika  nyuga mbalimbali,  ambapo huanzia
              akilini  mwa mtu kisha hudhihirika  kupitia  maumbo mbalimbali.  Katika uga
              wa fasihi, ubunifu hujitokeza kupitia maumbo kama vile shairi, insha, hadithi,
              riwaya, tamthiliya na utenzi. Watunzi wa kazi za fasihi huwa na kipaji, lakini
              wengine huwa watunzi bora kwa kujifunza. Kazi ya kubuni hutakiwa iwe na sifa
              kama vile: fikra za kisanaa kuhusu jambo au tukio; lengo au ujumbe maalumu;
              upya wa namna fulani; umuhimu kwa jamii, na izingatie maslahi na maadili ya
              jamii.


              Uandishi wa kazi za fasihi ni mchakato wa kiubunifu. Katika kuandika kazi za
              fasihi,  msanii  au  mwandishi  huanza  kwa  kujiuliza  maswali  kadha  wa  kadha.
              Baadhi  ya maswali  hayo ni:  Anaandika  kuhusu nini?  Anamwandikia  nani?
              Anaandika kwa kutumia mandhari ipi? Lengo lake ni nini? Na, anaandika kwa
              namna  gani?  Kwa kuwa  mwandishi  huandika  kazi  yake  ili  isomwe  na  watu
              wengine, hana budi kuzingatia mahitaji na mitazamo ya wasomaji wake ili aweze
              kuwapeleka anakotaka huku wakiendelea kufurahia kusoma kazi husika.

              Waandishi wa kazi za fasihi huandika kazi zao kwa malengo tofauti. Miongoni
              mwa  malengo hayo ni  kusawiri  uhalisi  wa kijamii ili  kuurekebisha  au  hata
              kuubadili ikibidi. Hii ina maana kuwa mwandishi sharti aibuke na vitu vipya
              ambavyo vitawavutia wasomaji katika kuwahabarisha yale yanayotokea katika
              jamii yao. Vilevile, waandishi wa kazi za fasihi huandika kwa lengo la kuelezea
              hisia zao ambazo wanaamini kuwa zitawavutia  wasomaji wao ili wayaone
              maisha kama wanavyoyaona wao. Pia, waandishi wanaandika ili kuwaburudisha
              wasomaji  wao. Hii inatokana  na ukweli  kuwa katika  mchakato  wa usomaji,
              msomaji hupata maarifa  na burudani. Halikadhalika,  waandishi huandika ili
              kuwashawishi wasomaji  wao wakubali  ukweli na namna  ya kufasili  mambo
              mbalimbali kama wanavyofanya wao. Mbali na hayo, waandishi huandika kwa
              lengo la kujipatia fedha kutokana na mauzo ya kazi hizo. Baadhi ya waandishi
              huandika ili watambuliwe na jamii zao.





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           143
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   143                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   143
   149   150   151   152   153   154   155   156   157   158   159