Page 149 - Fasihi_Kisw_F5
P. 149

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                           mimi  kama  dhahabu iliyo  katikati  ya mchanga.
                                           Pili, ni uzoefu nilioupata katika kufundisha somo
                                           la Kiswahili katika shule za sekondari wakati wa
                                           mafunzo  kwa vitendo  na wakati  wa ufundishaji
          FOR ONLINE READING ONLY
                                           wa kujitolea baada ya kuhitimu masomo yangu ya
                                           elimu ya juu.

                   Mjumbe 2:                Una ahadi au matumaini  gani ya kipekee
                                           unayotupatia ikiwa tutakuajiri?


                   Nagona:                   Ninaahidi  kuigeuza  taasisi  hii  kuwa kijiji  imara
                                           cha wataalamu wa Kiswahili.


                   Mjumbe 3:                Kufanya kazi katika taasisi kama hii kuna
                                           changamoto nyingi. Je, unazifahamu changamoto
                                           hizo? Na umejiandaaje kuzikabili?

                   Nagona:                   Ninatambua kuwa taasisi kama hii ambayo
                                           hujumuisha  watu  wengi  lazima  itakuwa  na
                                           changamoto. Mfano wa changamoto hizo ni kuwapo
                                           kwa akili na mitazamo tofauti ya kuyakabili masuala
                                           kadha wa kadha, wingi wa mambo yanayotokea,
                                           na masuala  mengine  yanayoendana  na  tabia  za
                                           watu. Hata hivyo, nimewahi kusoma riwaya
                                           moja iitwayo Kusadikika ambayo mhusika wake
                                           mkuu, Karama, alinifundisha  kuwa mapambano
                                           ya maisha yanahitaji vitu vikubwa vitatu ambavyo
                                           ni ubongo wenye utulivu, ulimi wenye staha, na
                                           moyo wenye ujasiri na saburi. Ninalihakikishia
                                           jopo hili kuwa nitatumia zana hizo tatu kukabiliana
                                           na changamoto  zitakazotokea  hapa. Ijapokuwa
                                           natambua kuwa si kazi rahisi, bali penye nia pana
                                           njia, hivyo ninatia nia ya kufanikiwa kuzikabili.

                   Mjumbe wa 4:             Bi. Nagona una matarajio gani kuhusu kiasi cha
                                           mshahara kama ukipata kazi hii?

                   Nagona:                   Ninashukuru sana kwa swali hili. Matarajio yangu
                                           ni kulipwa kufuatana na viwango vya mishahara
                                           vinavyoendana na ujuzi na elimu yangu.



               138                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   138                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   138
   144   145   146   147   148   149   150   151   152   153   154