Page 151 - Fasihi_Kisw_F5
P. 151

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (iii)  Nafasi ya lugha ya Kiswahili katika kukuza uchumi wa taifa

              (iv)  Dhima ya lugha ya Kiswahili katika kuleta umoja wa Afrika ya Mashariki.
              Kutumia maarifa ya kifasihi kuwasilisha hoja zenye mantiki na ushawishi
              katika malumbano ya hoja
          FOR ONLINE READING ONLY
              Malumbano ya hoja ni jukwaa muhimu katika kuwasilisha masuala mbalimbali.
              Vilevile,  ni nafasi nzuri ya kukuza maarifa  ya kujenga hoja zenye mantiki
              na ushawishi. Katika ulimwengu  wa kidijiti,  malumbano  ya hoja yanaweza
              kufanyika kwa kutumia vyombo vya habari kama vile runinga, redio na majukwaa
              ya mtandaoni. Wahusika hupeana mada kwa ajili ya kufanya maandalizi (yaani
              kuandaa  taarifa za msingi, ushahidi na kupangilia  mawazo  kimantiki),  kisha
              hukutana kwa ajili ya uwasilishaji. Kwa kawaida, hoja huwekwa mezani kisha
              kila mmoja hutoa mawazo yake kulingana na uelewa wa hoja hiyo. Ni muhimu
              kupeana nafasi wakati wa uchangiaji wa mawazo ili kuruhusu maelewano na
              kuheshimu mawazo ya mwingine katika mjadala. Vilevile, malumbano ya hoja
              huongeza maarifa ya usikivu.


               Shughuli ya 5.14
              Andaa hoja zenye  mantiki na ushawishi unazoweza  kuziwasilisha  katika
              malumbano ya hoja kuhusiana na mada yoyote kwa kutumia maarifa ya kifasihi.


                Tamrini

                 1.   Kwa kutumia mifano, fafanua mbinu zinazotumika kujenga ujumi.

                 2.   “Kujenga hoja kimantiki hakuna tija yoyote” Jadili hoja hii kwa mifano
                     thabiti.


                 3.   Eleza  namna utakavyojenga hoja zenye mantiki  na ushawishi kwa
                     kutumia misingi ya kifasihi.
                 4.   Fafanua namna misingi ya kifasihi inavyoweza kutumika kutathimini
                     matendo ya wahusika katika kazi ya fasihi.


                 5.   Kwa kutumia  mada  ya  ‘athari  za  dawa  za  kulevya kwa watoto  wa
                     mtaani’, andaa hoja zenye mantiki na ushawishi.

                 6.   Tumia misingi ya kujenga hoja zenye mantiki kutathmini maudhui ya
                     simulizi yoyote.





               140                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   140                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   140
   146   147   148   149   150   151   152   153   154   155   156