Page 146 - Fasihi_Kisw_F5
P. 146

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari



                   Mlinzi II:         (Anamkamata mwari 2) Nimekukamata  sasa … kwa
                                    nini ukaniendesha mbio? Kwa nini unanitimua? Tazama,
                                    unaona n’navyohema hivi? Pumzi juujuu, kwa nini?
                                    Mmekuwa kama  mang’ombe  yaliyovunja  zizi  kwa njaa
                                    na kiu ilhali mnashiba? Kwa nini hamtaki kushiba utulivu
          FOR ONLINE READING ONLY
                                    wa  miaka  mingi  uliopo  Giningi?  Kwa  nini  mnaona  kiu
                                    kwenye maji safi? Nyinyi waharibifu …

                   Mwari II:          Mchana ni mchana na usiku ni usiku; na ikiwa kumekucha
                                    basi  kumekucha;  asemaye  bado  ni  usiku  wa  manane  ni
                                    mwongo …

                   Mlinzi III:        Nani  mwongo hapa  enh? (Anamwelekeza  nalo  rungu,
                                    lakini mwari anarudi nyuma)

                   Mwari III:       Haijapata kutokea fujo hapa Giningi. (Huku akimfukuza
                                    … Mwari III anapiga kelele)

                   Mlinzi IV:       Mmekula … mmeshiba;  mmelishwa  sumu nini  nyinyi?
                                    Sumu gani? Na nani? Ah, mnataka kutwambia nini sasa?
                                    Mnataka kutwambia kwamba kuanzia leo jua halitatoka
                                    Magharibi na kuzama Mashariki? Mnataka kutwambia
                                    kwamba mchana kuna jua na usiku kuna kiza? Nani kasema
                                    hayo? Mmejigeuza watume wapya nyinyi mnakuja kuleta
                                    wahyi mpya hapa Giningi? Ah, wako wapi wafalme wetu
                                    wa Giningi? Nyinyi …

                   Mwari IV:        Ndiyo … tunasema  ndiyo, sote  kwa umoja  wetu, sasa
                                    tunaliona jua halitoki Magharibi: jua linatoka Mashariki
                                    na kuchwea Magharibi; hiyo ndiyo kanuni ya mwenendo
                                    wa jua enzi na azali! Ulimwenguni kote… na … na …
                                    (Anahema) usiku usio mbalamwezi na nyota ni kiza …
                                    kiza kitupu … na mchana usiyo mawingu ni mwangafu
                                    kwa jua linalodanda …

                   Mlinzi V:        Ngoja utaona … (Kwa mwari V)


                   Walinzi  na  wari  wengine  wanaingia  na  kutoka  na  sauti  za mabishano
                   zinazopandana na kuingiliana huku wakifukuzana na zogo na ghasia …


                                   Kivuli kinaishi (Mohamed, 2009:103-104)


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           135
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   135                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   135
   141   142   143   144   145   146   147   148   149   150   151