Page 156 - Fasihi_Kisw_F5
P. 156

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Muktadha wa kijiografia hujumuisha vipengele kama vile: sura ya nchi, uoto,
              bahari, maziwa, mito, na hali ya hewa. Vipengele hivi vina nguvu ya kushawishi
              kuandika kazi ya fasihi. Aghalabu, kazi zinazotokana na msukumo wa kijiografia
              husawiri masuala ya mazingira. Mwandishi anaweza kutunga hadithi, mashairi,
              riwaya au tamthiliya zinazojadili masuala ya viumbe hai na mazingira ya asili
          FOR ONLINE READING ONLY
              kulingana na uzoefu wake.

              Mbali na miktadha hiyo, uandishi wa kazi za kifasihi, kwa kiasi kikubwa,
              huchochewa  na  maisha  ya  mwandishi  na  uzoefu  wake  binafsi.  Mambo  haya
              huibua  hisia, matukio  muhimu  maishani,  na changamoto  anazokutana  nazo
              mwandishi. Hayo yote humchochea mwandishi kuandika utungo wa kiubunifu
              ili kuyawasilisha kwa wengine. Hata hivyo, licha ya kuwa kila mwandishi ana
              vyanzo vyake vya kipekee vinavyomchagiza kuandika kazi za fasihi ni muhimu
              kujifunza kutoka kwa wengine, na wakati huohuo kudumisha msukumo wa ndani
              wa kuandika ili kuendeleza uwezo wake wa kiubunifu katika uandishi wa kazi
              za kifasihi.

                                Zoezi la 6.1


                 1.   Eleza maana ya kutunga kazi changamani za kifasihi.

                 2.   Jadili dhana ya muktadha katika utunzi wa kazi za kifasihi.

                 3.   “Fasihi ni zao la kisiasa”. Jadili kauli hii kwa mifano thabiti.

                 4.   Fafanua namna masuala ya kijamii yanavyochagiza utunzi wa kazi za
                     kifasihi.


                 5.   Jadili namna utunzi wa kazi za kifasihi unavyoweza kuchochewa na
                     muktadha wa kiutamaduni.



               Shughuli 6.2
              Tumia maktaba na vyanzo vya mtandaoni, eleza fursa mbalimbali zinazotokana
              na kazi za kifasihi za Kiswahili.


              Fursa zinazotokana na kazi za kifasihi
              Ubunaji  wa  kazi  za  kifasihi  unatoa  fursa  nyingi  ambazo  humwezesha  msanii
              binafsi, kikundi na mashirika kukuza kipato kutokana na mchakato wa kuhariri,
              kuchapisha, kusambaza, na kuuza kazi za kifasihi. Vilevile, uandishi wa kazi za



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           145
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   145                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   145
   151   152   153   154   155   156   157   158   159   160   161