Page 159 - Fasihi_Kisw_F5
P. 159

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Mchango wa TEHAMA katika kukuza fursa za utunzaji, usambazaji,
              usomaji na uuzaji wa kazi za fasihi
              Matumizi ya TEHAMA yamechangia sana katika kutambua fursa mbalimbali
              zinazotokana  na  kazi  za  fasihi.  Ufuatao  ni  mchango  wa  TEHAMA  katika
          FOR ONLINE READING ONLY
              kutambua fursa hizo:

              Mosi, TEHAMA ina mchango mkubwa katika kuchambua kazi za fasihi. Hii
              inatokana na matumizi ya programu mbalimbali kama vile akili unde ambayo
              hutumika katika kuchambua kazi za fasihi simulizi na andishi.


              Pili, imewezesha uhifadhi na usambazaji wa kazi mbalimbali za kifasihi kwa
              urahisi  na  haraka  kupitia  mitandao  ya  kijamii.  Kutokana  na  hilo,  hadhira
              imekuwa ikitumia mitandao hiyo kusoma kazi hizo na kupata maarifa mbalimbali
              yanayohusiana na kazi za fasihi.


              Tatu, imesaidia kukuza hali za kiuchumi za watunzi kutokana na baadhi ya kazi
              hizo kuwekwa mitandaoni na kuwataka wasomaji kuzilipia kabla ya kuzipakua
              ili kuzisoma au kuzisikiliza.


              Nne, imechangia kukuza usomaji wa kazi za kifasihi kupitia vyanzo mbalimbali
              vya mtandaoni.  Wasomaji hufungua programu mbalimbali  ambazo  huzisoma
              wakati wowote na mahali popote na kujipatia maarifa kutoka katika kazi za fasihi
              ya Kiswahili.


              Tano,  TEHAMA imerahisisha  mawasiliano  kwa sababu imewaunganisha
              waandishi kwa kutumia majukwaa mbalimbali ya mitandao katika utendaji wao.
              Majukwaa hayo ni kama vile, makundi ya WhatsApp na majukwaa mbalimbali
              ya majadiliano. Majukwaa haya yamewezesha waandishi hao kushirikiana katika
              kazi za uandishi na usambazaji wa kazi zao kwa urahisi.

              Kwa ujumla, TEHAMA ina mchango mkubwa katika kuleta fursa mbalimbali
              kwenye fasihi ya Kiswahili kwa kutoa njia za utunzaji, usambazaji, usomaji na
              uingizaji wa kipato kwa watumiaji wa kazi za fasihi andishi.


               Shughuli ya 6.4
              Eleza jinsi TEHAMA inavyoweza kutoa fursa za kubidhaisha kazi ya kifasihi.










               148                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   148
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   148                   23/06/2024   17:54
   154   155   156   157   158   159   160   161   162   163   164