Page 158 - Fasihi_Kisw_F5
P. 158

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              na kuboresha stadi za uandishi. Vilevile, mhariri atakuwa na nafasi ya kushirikiana
              na wahariri wengine katika kuboresha kazi mbalimbali.

              Aidha, kazi za fasihi hutoa fursa ya kukuza na kuendeleza sanaa. Hii ni kutokana
              na kuwepo kwa watu wenye vipaji na hata kujifunza kutoka kwa wengine kwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              sababu ya kuangalia tamthiliya mbalimbali za ndani na nje ya nchi. Fursa hii
              huwawezesha watu kuingia katika ulimwengu wa sanaa na kujipatia  kipato.
              Fursa nyingine ya kisanaa ni kuwa mchoraji katika kazi mbalimbali za kifasihi,
              na vitabu vya watoto.


              Fursa nyingine itokanayo na uandishi wa kazi za fasihi ya Kiswahili ni kuwa
              mwalimu wa kuifundisha fasihi hiyo. Mwalimu humwezesha mwanafunzi
              kujenga misingi ya fasihi ya Kiswahili na kuwahamasisha wanafunzi kupenda
              kujisomea kazi mbalimbali za fasihi. Kadhalika, kazi za fasihi hutoa fursa ya
              kuwa mwalimu wa kufundisha masuala ya uandishi wa kazi bunifu. Kazi hizo
              za  kibunifu  zinaweza  kuwa za  hadithi/hadithi  za  watoto,  riwaya,  tamthiliya,
              mashairi, na insha za kifasihi.

              Kazi za fasihi humwezesha mtu kupata fursa ya kutafsiri vitabu vya fasihi. Tafsiri
              hizi huweza kuwa za vitabu vilivyoandikwa kwa lugha za Kiafrika na lugha za
              kigeni kwenda lugha ya Kiswahili na kinyume chake. Tafsiri hizo sharti zifanywe
              na mtu ambaye ana ujuzi wa kazi za fasihi ili kufumbata vionjo vya kifasihi
              katika lugha lengwa. Mfano wa vitabu vilivyotafsiriwa ni pamoja na tamthiliya za
              Mabepari wa Venisi, Juliasi Kaizari, Mfalme Edipode na Nitaolewa Nikipenda;
              na riwaya ya Barua Ndefu Kama Hii. Vitabu vilivyotafsiriwa huingia kwenye
              ushindani wa kibiashara, hivyo huingiza kipato kwa mtafsiri.


              Utunzi wa kazi za kifasihi humwezesha mtunzi kuwa mtafiti wa lugha na fasihi
              ya  Kiswahili.  Kupitia  utafiti  mtu  hujijengea  ujuzi  wa  mitindo  mbalimbali  ya
              uandishi wa kazi za kifasihi.


              Kimsingi, kazi za fasihi ya Kiswahili hutoa fursa nyingi kwa jamii. Fursa hizo ni
              kama za uaimbaji, uchoraji, uhariri, ualimu/uhadhiri, utafiti na uigizaji. Kazi zote
              hutoa fursa za kujipatia kipato na kukuza uchumi binafsi na wa nchi.


               Shughuli ya 6.3
              Kwa kutumia majukwaa ya kidijiti kama vile Instagram, WhatsApp na Youtube
              eleza mchango wa TEHAMA katika kuongeza fursa za kutangaza na kuuza kazi
              za fasihi.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           147
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   147                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   147
   153   154   155   156   157   158   159   160   161   162   163