Page 161 - Fasihi_Kisw_F5
P. 161

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kuandikia.  Vilevile,  mtunzi  anapaswa  kusoma  kazi  za  utanzu  husika,  kuteua
              hadhira, kuandaa vifaa atakavyohitaji, na kuandaa ratiba ya kazi. Kisha, anatakiwa
              kuandika dondoo muhimu za kazi. Ufuatao ni ufafanuzi wa vipengele hivi

              (b)  Kubuni wazo au mada
          FOR ONLINE READING ONLY
              Uandishi wa kazi ya fasihi hujengwa katika wazo kuu ambalo ndilo huchanuza
              mawazo madogomadogo ili kufikisha ujumbe kwa hadhira husika. Mtunzi wa kazi
              ya fasihi anapaswa kubuni wazo au mada itakayowavutia wasomaji na kuwapa
              hamasa ya kusoma kazi yake. Mada au wazo hilo linaweza kuwa la kufikirika, la
              kihistoria au mada inayohusu masuala muhimu ya kijamii. Mwandishi anaweza
              kupata wazo kutokana na uzoefu wake au mambo aliyoyapitia katika maisha
              na  miktadha  mingine.  Vilevile,  anaweza  kufanya  utafiti  ili  kuelewa  masuala
              yanayogusa jamii yake, ambayo yatamsaidia kupata wazo la kuandikia. Mambo
              yanayoigusa  jamii  yanaweza kuwa ya kijamii,  kisiasa, kiuchumi  na masuala
              mtambuka.  Ni  vizuri  mwandishi  abuni  mada  anayoipenda  na  atakayoimudu
              kuiandikia kazi yake.

              (c)  Kufanya uchunguzi
              Baada ya kupata wazo au mada, mtunzi anaweza kukusanya taarifa anuai kuhusu
              wazo alilolipata. Anaweza kusoma vitabu, makala, au hata kufanya utafiti kuhusu
              wazo hilo. Lengo ni kupata maarifa ya kutosha na taarifa sahihi kuhusu wazo/
              mada.  Vilevile, uchunguzi humwezesha  mtunzi  kuelewa  mazingira  ya jamii,
              historia, utamaduni, na masuala  mengine  yanayohusiana na wazo au mada
              iliyochaguliwa.

              (d)  Kuamua kuhusu utanzu wa kuandika
              Kila utanzu huwa na mtindo wake wa kiuandishi. Kwa hiyo, mtunzi anapaswa
              kuamua kuhusu utanzu atakaoutumia  katika kuwasilisha wazo au mada
              aliyoibuni. Utanzu huo unaweza kuwa wa ushairi, tamthiliya, hadithi au riwaya.
              Hii itamsaidia kufikisha ujumbe wake kwa kuzingatia muundo na mtindo wa
              kiuandishi wa utanzu husika. Kwa mfano, ikiwa ni mashairi, mtunzi atapaswa
              kuzingatia kaida mbalimbali za ushairi kama vile: muundo, mtindo, lugha ya
              kishairi na mambo mengine yanayohusu ushairi. Ni vyema mwandishi akaandikia
              utanzu anaoumudu.

              (e)  Kusoma kazi za utanzu husika
              Usomaji wa kazi husika za fasihi humpa mwandishi fursa ya kujifunza kutoka
              kwa waandishi wengine, ili kupata maarifa na kuimarisha stadi ya kuandika. Pia,
              humsaidia mtunzi kuwa na uelewa mzuri wa vipengele vya uandishi kama vile




               150                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   150                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   150
   156   157   158   159   160   161   162   163   164   165   166