Page 164 - Fasihi_Kisw_F5
P. 164

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari





                                Zoezi la 6.3


                 1.   Jadili kauli kuwa “uandishi wa kazi za kifasihi ni mchakato usiohitaji
                     utaratibu”.
          FOR ONLINE READING ONLY
                 2.   “Maandalizi  ni hatua muhimu kabla ya uandishi wa kazi ya fasihi”.
                     Jadili.

                 3.   Kwa kutumia mifano eleza masuala muhimu ambayo hufanyika katika
                     hatua ya kuboresha.

                 4.   Tofautisha hatua ya uhariri na ya mapitio ya mwisho katika utunzi wa
                     kazi za kifasihi.

                 5.   “Mapitio ya mwisho ni hatua inayompotezea muda mwandishi.” Jadili.


               Shughuli ya 6.7

              (a)  Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni,  maktabani  na vinginevyo,  eleza

                   maana na kanuni zinazoongoza utunzi wa maigizo.

              (b)  Angalia  au  sikiliza  maigizo  kutoka  katika  vyanzo  mbalimbali,  kisha
                   chambua kanuni zilizotumika katika utunzi wa igizo mojawapo.

              Kanuni za kutunga maigizo, mashairi na hadithi za watoto
              Utunzi wa kazi yoyote ya kifasihi huongozwa na kanuni maalumu  ambazo
              hutumika katika kutunga kazi za utanzu husika. Ufuatao ni ufafanuzi wa kanuni
              za kutunga maigizo, mashairi na hadithi za watoto.

              Kanuni za kutunga maigizo
              Maigizo ni kipera cha sanaa za maonesho ambacho ni miongoni mwa tanzu za
              fasihi simulizi. Maigizo ni  sanaa ya kuwasilisha jambo au tukio kwa kutumia
              lugha na vitendo. Mara nyingi maigizo hutendwa kwenye jukwaa la maonesho au
              mahali popote maalumu mbele ya hadhira husika. Maigizo yanahitaji kutungwa
              kwa ustadi ili kuwakonga watazamaji. Hatua za utunzi wa maigizo kwa kiasi
              kikubwa zinafanana na zile za utunzi wa kazi nyingine za kifasihi isipokuwa
              utunzi wa maigizo hujumuisha vipengele  muhimu vinavyopatikana  katika
              maigizo tu. Kanuni muhimu za kuzingatiwa katika utunzi wa maigizo ni pamoja
              na hizi zifuatazo:




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           153
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   153                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   153
   159   160   161   162   163   164   165   166   167   168   169