Page 162 - Fasihi_Kisw_F5
P. 162

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              lugha,  mtindo, na muundo unaotumiwa  katika  utanzu  husika. Kufanya hivyo
              humwongezea mtunzi maarifa ya namna ya kuandika kazi yake.

              (f)  Kuteua hadhira
              Mwandishi huandika  kazi yake  ili  iweze  kusomwa  na jamii.  Kwa mantiki
          FOR ONLINE READING ONLY
              hiyo, hana budi kujua aina ya watu anaowaandikia kazi husika. Mwandishi
              anatakiwa kujua mahitaji ya wasomaji wake, ikiwamo mitazamo yao kuhusu kile
              anachokiandikia. Kwa mfano, kama mwandishi anawaandikia watoto, anatakiwa
              kuandika kwa kutumia lugha nyepesi itakayowawezesha kuelewa maudhui hayo
              kwa urahisi. Aidha, anaweza kuweka picha au michoro yenye rangi mbalimbali
              ili kuwavutia watoto na kuwajengea kumbukumbu.

              (g)  Kuandaa zana
              Katika  hatua  hii,  mwandishi  anaweza  kubainisha  vifaa  na  mahitaji  mengine
              ambayo yatamsaidia kuandaa kazi husika, zikiwamo shajara, kompyuta na simu.
              Pia, mwandishi anaweza akaandaa ratiba ambayo itamwongoza katika mchakato
              wote wa kuandika kazi yake kulingana na utanzu anaouandikia.

              (h)  Kuandika madondoo ya utunzi
              Mwandishi anapaswa kuandika dondoo kuhusu sehemu muhimu za kazi yake.
              Dondoo hizo, ambazo zitamwongoza katika uandishi wake, zinaweza kujumuisha
              vipengele vya: majina ya wahusika wakuu, majina ya wahusika wengine,
              mandhari, dhamira mbalimbali anazokusudia kuziwasilisha, mtindo wa uandishi
              na mpangilio wa visa na matukio.


              (i)  Kuandika/kutunga
              Baada ya kufanya maandalizi  ya uandishi, mwandishi anapaswa kuanza
              kuandika kazi yake kwa kuzingatia  dondoo au mwongozo aliouandaa.  Hapa
              ndipo anapoweka mawazo yake katika  maandishi  kwa kuumba wahusika,
              visa na matukio yanayosawiri wazo lake la ubunifu. Vilevile, katika hatua hii,
              mwandishi hapaswi kuhofia makosa yoyote ya lugha bali aruhusu mtiririko wa
              mawazo kwa mawanda mapana ili kukamilisha rasimu ya kwanza. Anatakiwa
              kupangilia mawazo vizuri ili kuleta mantiki katika visa na matukio. Mawazo
              au dhamira ndogondogo ni lazima zijengane na dhamira kuu. Aidha, mwandishi
              aepuke kujaza mawazo ambayo hayana tija katika kazi yake. Hii inamaanisha
              kwamba kila kinachoandikwa kiwe kinalenga kuiendeleza au kuikamilisha kazi.
              Kadhalika, ahakikishe anawaumba vizuri wahusika ili kusawiri migogoro. Aidha,
              atumie lugha ya kisanaa iliyojaa taswira, tamathali za usemi na mbinu nyingine
              za kifasihi.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           151
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   151                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   151
   157   158   159   160   161   162   163   164   165   166   167