Page 165 - Fasihi_Kisw_F5
P. 165

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (a)  Wazo au mgogoro
              Igizo lolote,  kama kazi yoyote ya sanaa, lazima  liwe na wazo au mgogoro
              unaovutia au wenye uzito. Mgogoro ni tatizo ambalo linahitaji utatuzi.


              (b)  Msuko wa matukio au matendo
          FOR ONLINE READING ONLY
              Hatua ya pili ya utunzi wa igizo ni uteuzi wa matukio yaliyopangiliwa katika
              mfuatano wa usababishano – tukio moja likisababisha jingine, toka mwanzo
              hadi mwisho. Msuko wa matukio unapaswa kuibua msisimko na taharuki kwa
              wasikilizaji na watazamaji. Matukio haya huteuliwa na mtunzi lakini yanaweza
              kubadilishwa katika uigizaji jukwaani.

              (c)  Matumizi ya dayalojia
              Mazungumzo  katika  maigizo  hayaandikwi,  bali  huibuka  kulingana  na
              makubaliano baina ya waigizaji, na kufuata matukio yaliyopangwa.


              (d)  Wahusika
              Wahusika  katika  maigizo  wanatakiwa  kuumbwa  kwa  kuzingatia  mahitaji  ya
              vitendo husika. Wanatakiwa kuvutia, wawe wa kipekee na wauvae uhusika vizuri
              ili kufanya uigizaji kuwa hai na kuhamasisha hisia kwa hadhira. Majukumu ya
              wahusika yanatakiwa kuwa wazi na yanayoendana na dhamira ya igizo. Wahusika
              kinzani huongeza msisimko na mvuto katika maigizo kwa sababu huchochea
              migogoro, na migogoro ndiyo inayosukuma simulizi.

              (e)  Mandhari
              Ijapokuwa mandhari ya igizo yanapaswa kuwa ya kuaminika na yenye uhalisi
              ili kuendana na tukio, kuna maigizo yenye mandhari za kufikirika. Kwa jumla,
              mandhari ya igizo inayovutia na iliyoundwa na mazingira ya kipekee, hufanya
              simulizi ya igizo kuwa na nguvu ya ushawishi zaidi.

              (f)  Kugusa hisia za hadhira
              Kazi ya maigizo ikisukwa vizuri huibua hisia na misisimko ya aina nyingine kwa
              hadhira  husika. Mwandishi anayegusa  hisia za hadhira  ndiye husemwa kuwa
              kafanikiwa sana katika utunzi wake.


              Ikumbukwe  kuwa  utunzi  wa  maigizo  si  wakuandika  bali  ni  wa kuzungumza
              na kutenda wazo kwa mujibu wa mfuatano  mahususi wa matukio.  Maigizo
              hayasomwi bali husikilizwa na kutazamwa.

               Shughuli ya 6.8
              Chagua suala moja mtambuka, kisha tunga igizo kwa kuzingatia kanuni za utunzi.



               154                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   154
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   154                   23/06/2024   17:54
   160   161   162   163   164   165   166   167   168   169   170