Page 167 - Fasihi_Kisw_F5
P. 167

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (f)  Utoshelevu
              Ni muhimu shairi liwe na mtiririko mzuri wa mawazo unaolandana na mpangilio
              wake. Mpangilio huo ndio unaoleta utoshelevu. Utoshelevu ni kanuni ambayo
              inautaka kila mshororo na kila ubeti kujitosheleza kimaana ili kulifanya shairi
          FOR ONLINE READING ONLY
              likamilike kifani na kimaudhui.
               Shughuli 6.10

              (a)  Soma mashairi mawili kutoka katika diwani teule kisha chambua kanuni
                   zilizotumika katika utunzi wake.


              (b)  Chagua mada unazozipenda kisha tunga mashairi mawili yasiyopungua beti
                   kumi (10) kwa kila shairi.
               Shughuli ya 6.11

              (a)  Chunguza vitabu teule vya hadithi za watoto, kisha eleza maana na sifa za

                   hadithi hizo.

              (b)  Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni,  maktabani  au kwingineko, jadili
                   kanuni za utunzi wa hadithi za watoto.

              Kanuni za kutunga hadithi za watoto
              Hadithi za watoto ni aina ya kazi za fasihi zilizobuniwa kwa ajili ya watoto. Visa
              na matukio, lugha, wahusika, michoro na picha, na maudhui yanayowasilishwa
              katika hadithi za watoto huakisi hisia na akili za watoto. Hadithi hizi huwa na
              sifa ambazo ni tofauti na hadithi za watu wazima ama hadithi nyingine. Hadithi
              za watoto huweza kuwa na maandishi yenye ukubwa tofauti kulingana na umri
              wa watoto, utofauti wa nafasi kati ya mstari na mstari, nakshi ya rangi, picha na
              michoro, kurasa chache, lugha rahisi na wahusika wachache kulingana na umri
              wa watoto.

              Licha ya upekee wa hadithi za watoto lakini hatua za uandishi huwa ni sawa na
              za kazi nyingine za kifasihi. Vilevile, vipengele vinavyojenga hadithi za watoto,
              kama vile, lugha, wahusika, msuko wa visa na matukio huwa sawa na kazi
              bunilizi nyinginezo kama vile hadithi fupi na riwaya. Pamoja na mfanano huo,
              utunzi wa hadithi za watoto huongozwa na kanuni zifuatazo:

              (a)  Lugha
              Hadithi  za  watoto  hutumia  lugha  rahisi,  inayoeleweka  na  ya  kisanaa.  Sanaa
              katika lugha ya watoto hujumuisha semi, tamathali za semi na methali kulingana



               156                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   156
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   156                   23/06/2024   17:54
   162   163   164   165   166   167   168   169   170   171   172