Page 171 - Fasihi_Kisw_F5
P. 171

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                               Faharasa

              Akili mnemba:        Mfumo wa kidijiti ambao umetengenezwa kwa ajili ya kutoa
                                 majibu ya masuala mbalimbali
          FOR ONLINE READING ONLY
              Buni:              Gugundua au tengeneza kitu kwa mara ya kwanza

              Falsafa            Elimu kuhusu asili, maana na sababu za mambo au vitu
              Fani:              Ufundi anaoutumia msanii katika kuwasilisha maudhui

              Fantasia:            Wazo la kufikirika lisiloweza kutekelezeka
              Fumbo:               Usemi au kauli  ambayo  maana  yake haitolewi  waziwazi  bali
                                 hufichwa

              Fursa:             Nafasi ya kuweza kufanya jambo
              Futuhi:            Aina ya tamthiliya inayokusudia kufurahisha au kuchekesha, na
                                 huwa na mwisho mwema (Pia, ramsa)
              Hadithi fupi:        Simulizi  ya kubuni inayosawiri  tukio, tabia,  mgogoro au
                                 kipengele fulani cha maisha kwa ufupi, kwa kawaida, hadithi
                                 fupi huwa na tukio moja au mawili na hutumia mawanda finyu
              Hadithi za watoto:  Tungo za kibunifu zinazowahusu watoto kifani na kimaudhui

              Hadithi:           Matukio  yanayosimuliwa  kwa mfuatano  wa kimantiki  na
                                 kiwakati
              Hekaya:            Ngano zenye visa visivyo vya kawaida vinavyoambatana  na
                                 masaibu  na pengine  hata  ujanja  wa mhusika  mkuu ambaye
                                 huweza kuwa mtu au mnyama

              Hurafa:            Ngano zenye wahusika wanyama tu ambao huwakilisha tabia na
                                 matendo ya binadamu kwa kurejelea masuala yanayopatikana
                                 katika jamii ili kuwasilisha maana

              Insha:             Utungo mfupi  wa kinathari  (wa lugha  ya  mjazo)  ambao
                                 husimulia jambo kwa utimilifu
              Istiara:           Hadithi ambayo maana yake ya wazi inawakilisha  maana
                                 iliyofichika.  Kwa  hiyo,  maana  huwasilishwa  kwa  njia  ya
                                 mafumbo.

              Itikadi:           Jumla ya mfumo wa mawazo, fikra au imani inayoongoza na
                                 kumwelekeza mtunzi katika kuwasilisha masuala mbalimbali
              Jukwaa:            Eneo maalumu lililotengenezwa  kwa kuinuliwa juu ndani ya
                                 jingo, ukumbi au uwanja ambalo hutumika kwa kutolea hutuba
                                 au michezo

               160                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   160
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   160                   23/06/2024   17:54
   166   167   168   169   170   171   172   173   174   175   176