Page 175 - Fasihi_Kisw_F5
P. 175

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari



              Tafsiri:           Ni uhawirishaji wa mawazo yaliyoandikwa kutoka lugha moja
                                 hadi nyingine
              Tahakiki:          Andiko linalochambua na kufafanua kazi fulani ya fasihi

              Taharuki:          Hali ya kusisimua au wasiwasi kuhusu jambo fulani litakalotokea
          FOR ONLINE READING ONLY
                                 katika kipindi kijacho
              Takhmisa:          Shairi lenye mistari mitano
              Takriri:           Dhana inayotumika kuelezea hali ya kurudiarudia sauti, silabi,
                                 neno au maneno
              Tamthiliya:        Mchezo ulioandaliwa kwa lengo la kuigizwa jukwaani

              Tanakali lafudhi:   Tamathali inayotumika kuonesha mwigo wa matamshi ya watu
                                 fulani wanaotumia lugha kwa namna fulani

              Tanakali sauti:      Tamathali  inayotumika  kuonesha  mwigo  wa sauti  za  vitu
                                 mbalimbali kulingana na lengo na muktadha husika

              Taniaba:           Tamathali ambayo hutumia jina la mtu binafsi kwa watu wengine
                                 wenye tabia, mwenendo hali au kazi sawa na ya mtu huyo

              Tarbia:            Shairi la kimapokeo lenye mistari minne
              Tarihi:            Hadithi zinazohusu matukio muhimu ya kihistoria

              Tasdisa/Sudusia:   Shairi lenye mistari sita
              Tashibiha:         Tamathali inayotumika kuelezea hali ya ulinganishi kwa kutumia
                                 maneno ya ulinganishi kama vile kama, mithili ya, mfano wa, na
                                 sawa na

              Tashihisi:         Tamathali ambayo vitu visivyo na uhai na uwezo wa kutenda
                                 hupewa uwezo huo

              Tafsida:           Lugha ya staha yenye lengo la kupunguza ukali au matusi katika
                                 kauli

              Taswira:           Picha au jazanda inayojengwa akilini mwa hadhira anapoifuatilia
                                 kazi ya sanaa

              Tathlitha:         Shairi lenye mistari mitatu
              Tini:              Muhtasari wa kumbukumbu za hoja au mawazo zinazoandikwa
                                 kwa ajili ya kusomwa baadaye


              Ubunifu:           Uwezo wa kutafakari na kujenga fikra zinazounda na kufanya
                                 kitu au jambo jipya lionekane

              Uhakiki:           Dhana  inayohusika  na  kuchambua,  kufafanua,  kufasili,
                                 kutathmini, na kueleza vipengele vya fani na maudhui katika
                                 kazi za fasihi

               164                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   164
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   164                   23/06/2024   17:54
   170   171   172   173   174   175   176   177   178   179   180