Page 172 - Fasihi_Kisw_F5
P. 172

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari



              Kigano:            Hadithi fupi ya fasihi simulizi ambayo hutolewa kwa kutumia
                                 matumizi mapana ya ujadi

              Kipera:            Tawi la utanzu wa fasihi
              Kisa:              Masimulizi ya tukio la kweli lililotokea
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kisasili:          Hadithi  inayoaminiwa  kuwa kweli,  inayoelezea  chimbuko  au
                                 asili ya kitu na hufungamana na imani na miviga ya jamii
              Kisasuli:          Hadithi yenye kueleza usuli na sababu za jambo, tukio au hali
                                 (yaani kwa nini jambo, tukio au hali iko kama ilivyo). Kisasuli
                                 hakina uzito mkubwa kama kisasili, na si lazima kiaminiwe na
                                 wanajamii.

              Kitendawili:       Usemi mfupi wa mafumbo wenye kutumia  lugha ya picha,
                                 tamathali na ishara katika kueleza jambo lililofichika

              Lakabu:            Jina au majina ya nyongeza au ya kupanga (ambayo sio halisi)
                                 ambayo baadhi ya watu hupewa au hujipa kutokana na sifa zao
                                 za kimaumbile, kinasaba, kitabia, kiujuzi au kimatendo

              Lugha:             Njia ya mawasiliano ya kufikisha ujumbe uliokusudiwa. Mfano:
                                 lugha ya maandishi, lugha ya masimulizi, lugha ya ishara, lugha
                                 ya alama na lugha ya vitendo

              Maghani:           Tungo za kishairi zinazotongolewa kwa kutumia sauti iliyo kati
                                 ya uimbaji na uzungumzaji

              Maigizo:           Sanaa inayotumia watendaji kuiga tabia na matendo ya watu au
                                 viumbe wengine ili kuelimisha au kuburudisha
              Majazi:            Tamathali ya usemi ambayo wahusika wa kazi ya fasihi hupewa
                                 majina yanayoakisi wasifu au tabia zao
              Majigambo:         Masimulizi ya kujisifia au kujikweza kwa mtu kuhusu mambo
                                 anayoweza kuyafanya, aliyowahi kuyafanya au atakayoyafanya

              Makala:            Habari  iliyoandikwa  kueleza  jambo  mahususi  kwenye  gazeti,
                                 jarida au kitabu

              Maktaba:           Mkusanyo wa machapisho kama vitabu, kanda, yaliyohifadhiwa
                                 na ambayo huweza kuazimwa na kutumiwa
              Maleba:            Mavazi, vifaa na mapambo ya msanii anapokuwa jukwaani
              Mandhari:          Muonekano wa mahali unaojumuisha ardhi, miti, mito, milima
                                 au mabonde
              Maudhui:           Jumla ya mambo mbalimbali  yanayozungumziwa  katika  kazi
                                 ya fasihi ambayo yanajengwa na dhamira,  mtazamo,  falsafa,
                                 itikadi, msimamo, ujumbe, mafunzo na migogoro

                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           161
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   161                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   161
   167   168   169   170   171   172   173   174   175   176   177