Page 173 - Fasihi_Kisw_F5
P. 173

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Mdokezo:             Tamathali  ambayo  kitu  fulani  hudokezwa  au  huachwa  bila
                                 kukamilishwa, aghalabu, kitu hicho huwa kinafahamika katika
                                 muktadha husika
              Methali:           Semi za kimapokeo zenye hekima na busara zinazotumia sitiari
                                 kuelezea falsafa na uzoefu wa jamii fulani kwa muhtasari
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mgogoro:           Ni  hali  ya  watu  kukosa  kukubaliana  kuhusu suala  fulani
                                 inayoweza kusababisha mitafaruku
              Mhadhiri:          Mtaalamu au mwalimu wa taasisi ya elimu ya juu anayeelimisha
                                 watu kwa njia ya mhadhara
              Mhusika Bapa:        Mhusika ambaye habadiliki kulingana na wakati, mazingira au
                                 muktadha; yaani huonesha upande mmoja tu
              Mila:              Ni taratibu za kimaisha za mwenendo na jinsi ya kufanya mambo
                                 zinzofuatwa na jamii fulani kulingana na historia na utamaduni
                                 wao

              Misingi:           Chanzo au chimbuko la kitu fulani
              Mitandao ya kijamii:   Programu inayowezesha watu kuwasiliana kwa njia ya tovuti
                                    au mfumo mwingine wa mawasiliano ya kielekitroniki
              Miviga:            Sherehe au shughuli za kijadi zinazofanywa na jamii  katika
                                 kipindi maalumu cha mwaka au katika muktadha maalumu
              Mkondoni:          Kuwa katika hali ya kuunganishwa na mtandao kupitia kompyuta
                                 au vyombo vingine kidijiti
              Mleo:              mstari wa tatu wa shairi la beti za mistari mitatumitatu

              Mloto:             mstari wa pili katika ubeti wa shairi
              Mtandao:           Mfumo wa mawasiliano  ya kielektroniki  unaopitia  katika
                                 kompyuta ulimwenguni unaotumiwa kutafuta taarifa kuwasiliana
                                 au kupeana taarifa

              Mtazamo:           Namna au jinsi mtu anavyochukulia kitu au jambo kisiasa au
                                 kiuchumi

              Mtindo:            Kipengele cha kifani kinachohusu upekee au utofauti wa msanii
                                 unaojitokeza katika kazi ya fasihi na hutokana na matumizi ya
                                 lugha  na  vielelezo.  Mtindo humtofautisha  msanii  mmoja  na
                                 mwingine katika kazi moja na nyingine

              Muundo:            Kipengele cha kifani kinachohusu umbo au mwonekano wa kazi
                                 ya sanaa

              Mwandamizi:        Kipande au mgao wa tatu katika  mshororo wa shairi ambalo
                                 mishororo yake imegawanyika katika vipande vitatu





               162                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   162
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   162                   23/06/2024   17:54
   168   169   170   171   172   173   174   175   176   177   178