Page 139 - Fasihi_Kisw_F5
P. 139

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Maswali

                   (i)  Ni maana  zipi  unaweza  kuzipata  katika  mstari  usemao “Wataanza
                        kutalii mipaka mende usiku”?
          FOR ONLINE READING ONLY
                   (ii)  Ni taswira zipi unaweza kuzijenga kutokana na jina la shairi hili?

                   (iii)  Mstari usemao “Bila woga, bila ruhusa ulichonacho watakula”  una
                        maana zipi?
                   (iv)  Mstari usemao “Kifo cha mende sharti miguu juu” unamaanisha nini?

                   (v)  Ni njia zipi umezitumia katika kupata maana za mistari iliyodondolewa
                        katika maswali namba i, iii na iv?

                   (vi)  Ni maana zipi unaweza kuibua kutokana na shairi hili? Kwa nini?

              (c)  Soma mashairi mawili kutoka katika diwani teule, kisha, kwa uthibitisho wa
                   mifano, chambua maana na mbinu mbalimbali za kiujumi zinazopatikana

                   katika mashairi hayo.

              Maana zinazopatikana katika tamthiliya
               Shughuli ya 5.7

              (a)  Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.

                   Bi Moja:  Vipi habari ya safari. Mbona umerudi na vitambaa vyote?

                   Bi Tano:   Hakuna wanunuzi.

                   Wote:    Aah hata! Haiwezekani!

                   Bi Moja:  Hata haiwezekani! Sema tu hukwenda.


                   Bi Tano:   [Amekasirika]: Yaani mnasema mimi mvivu siyo?

                              Nimezunguka  mji  mzima  na  zigo  hilo halafu mnaniambia
                            mimi  mvivu? Nawaambia watu hawataki  kununua. Au mlitaka
                            niwagawie bure.

                   Bi Nne:    Lakini kwa nini wakatae kununua hivi, mbona vile vya mwanzo
                            walinunua?

                   Bi Moja:  Tena walikuwa wanavigombania.



               128                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   128
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   128                   23/06/2024   17:54
   134   135   136   137   138   139   140   141   142   143   144