Page 136 - Fasihi_Kisw_F5
P. 136

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   madhara  hutokea  duniani  kutokana  na uongo wa watu  wakubwa kuliko
                   ule  wa watu  wadogo. Ukitaka  kuwa mwongo lazima  usiwe msahaulifu.
                   Kutosahau  ni  jambo  lifikirikalo  lakini  haliwezekani.  Kwa  hivi,  njia  ya
                   mwongo fupi. Uongo ni kama giza, hukimbia mbele ya cheche ndogo ya
          FOR ONLINE READING ONLY
                   nuru ya kweli. “Uongo hukimbia kweli ikidhihiri” ni methali ya Kiswahili
                   ikumbushayo  watu udhaifu  wa uongo. Uovu mkubwa wa uongo ni  mtu
                   kujidanganya mwenyewe. Jambo kama hili hutokea mara kwa mara kwa
                   waongo. Muongo humcha mno mtu kuliko Mungu.


                                   Insha na Mashairi (Robert, 1967:1)
                   Maswali


                   (i)  Ni maana zipi zinapatikana katika sentensi isemayo “Bahari moja ya
                        hatari katika dunia ni uongo”?
                   (ii)  Msemo wa “Ukitaka kuwa mwongo lazima usiwe msahaulifu” una
                        maana zipi?

                   (iii)  “Tashibiha” iliyotumika katika insha hii ina maana gani?

                   (iv)  Ni maana zipi unaweza kuzipata katika sentensi ya “Baadhi ya madhara
                        hutokea duniani kutokana na uongo wa watu wakubwa kuliko ule wa
                        watu wadogo”?

                   (v)  Ni taswira zipi unaweza kuziibua kutoka katika insha hii?
                   (vi)  Ni maana zipi unaweza kuziibua kutokana na insha hii? Kwa nini?


              (b)  Soma insha ifuatayo,  kisha chambua  maana  mbalimbali  zinazopatikana
                   katika insha hiyo.

                                          URAFIKI WA PAKA
              Wanyama  katika  kuimarisha  maisha  yao,  hujenga  mahusiano  wao  kwa wao
              na kwa binadamu. Binadamu huwatumia wanyama hawa kwa shughuli kadha
              wa kadha. Wanyama wengine wana jukumu la kuleta burudani kwa binadamu
              kama vile gwaride, nyimbo, ngoma na vichekesho. Paka ni mmoja wa wanyama
              wenye urafiki na binadamu kutokana na mwenendo wake. Binadamu amekuwa
              akimwamini na kumpa kiti cha kushughulikia mambo mengi ofisini mwake.


              Sauti isikikayo mithili ya kinanda humpatia paka upekee wa ajabu. Akimwona
              mgeni huimba kwa sauti nyororo! Nyau! Nyaau! Nyaaau! Nyaaaau! Mlio wake



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           125
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   125                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   125
   131   132   133   134   135   136   137   138   139   140   141