Page 129 - Fasihi_Kisw_F5
P. 129

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   masimulizi, mavazi, vyakula, maudhui ya Kiafrika, pamoja na mienendo
                   mbalimbali ya Kiafrika.

              Uchambuzi wa mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika kazi za fasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
              Mbinu zinazotumika katika kujenga ujumi huweza kuchambuliwa katika kazi
              za kifasihi kama vile mashairi, tamthiliya na majigambo. Mbinu hizi za kifasihi
              huipa kazi  husika ujumi  ambao  humfanya  msomaji  au mtazamaji  kuvutiwa
              au kutokuvutiwa nao. Mbinu hizo hujitokeza  katika kazi za kifasihi kama
              inavyodhihirika katika shughuli zifuatazo:

              Mbinu zilizotumika kujenga ujumi katika mashairi

               Shughuli ya 5.2

              (a)  Soma shairi lifuatalo, kisha jibu maswali yanayofuata:


                               Kiswahili

                               Titi la mama li tamu, hata likiwa la mbwa,
                               Kiswahili naazimu, sifayo inayofumbwa,

                               Kwa wasiokufahamu, niimbe ilivyo kubwa,

                               Toka kama chemchemu, furika palipozibwa,

                               Titi la mama li tamu, jingine halishi hamu.




                               Lugha kama Kiarabu, Kirumi na Kiingereza,

                               Kwa wingi zimeratibu, mambo ya kupendeza,

                               Na mimi nimejaribu, kila hali kujifunza,

                               Lakini sawa na bubu, nikizisema nabezwa,

                               Titi la mama li tamu, jingine halishi hamu.













               118                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   118                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   118
   124   125   126   127   128   129   130   131   132   133   134