Page 128 - Fasihi_Kisw_F5
P. 128

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              wanakubaliana kwamba ujumi ni utambuzi wa uzuri au ubaya katika maumbile
              asilia, vitu aundavyo mtu na sanaa. Tajiriba za kiujumi zinazoibuliwa katika akili
              au hisia za mtu hujumuisha kuajabia au kufurahisha au kupendezewa au kuvutiwa
              kwa uzuri wake. Kipimo cha uzuri wa kitu hujengeka katika utambuzi (kiakili na
          FOR ONLINE READING ONLY
              kihisia) wa mtu katika makuzi au malezi yake. Kipimo hiki hakihusu uzuri tu bali
              pia ubaya wa kitu; na ubaya huu hujumuisha upungufu katika umbile au sanaa.

              Kama ilivyo kwa jambo au kitu chochote, kazi ya fasihi pia huweza kuonwa
              kama nzuri au mbaya. Watunzi huhakikisha kuwa kazi zao zinakuwa na thamani
              ya kiujumi, yaani hadhi na mvuto kwa hadhira. Watunzi hao huujenga ujumi
              kwa kutumia mbinu mbalimbali za kibunifu. Mifano ya mbinu hizo ni: taharuki,
              ufutuhi, utanzia, utomeleaji, ujenzi wa wahusika, usawiri wa mandhari pamoja
              na uteuzi na mpangilio mzuri wa maneno. Matumizi ya mbinu hizi huifanya kazi
              ivutie na iwe na upekee. Mbinu nyingine ya kujenga ujumi katika kazi ya fasihi
              ni kuzingatia vipengele vya kijadi. Watunzi hutumia ujadi katika vipengele kama
              vile majina au mandhari yanayojulikana na hadhira. Ujadi vilevile hutokana na
              uzoefu na tajriba ya hadhira. Mathalani, uzuri wa hadithi au ngano zenye mhusika
              sungura unatokana na kukidhiwa kwa matarajio  ya hadhira  kwamba lazima
              mhusika huyu atafanya ujanja fulani. Ikiwa mhusika huyu atatumika vinginevyo,
              hadhira inaweza isiuone uzuri wa hadithi au ngano uliozoeleka kijadi kuhusu
              ujanja wa sungura. Kufanya hivi kunaifanya hadhira ijione iko karibu sana na
              kazi. Mbinu nyingine ni kuzingatia uhalisi. Mtunzi anapotunga kazi inayoakisi
              mambo ya kweli yanayotokea katika jamii ya hadhira yake huifanya kazi iwe na
              thamani kwa hadhira hiyo. Zaidi, kazi hutakiwa kuzingatia maadili ya hadhira
              inayolengwa. Kazi inayoheshimu miiko au inayoepuka mambo yanayokatazwa
              na jamii huwa na thamani zaidi kwa hadhira kuliko inayokiuka maadili.

              Mbinu nyingine inayoweza kutumika ni ile ya mtazamo wa Kiafrika kuhusu
              ujumi.  Katika  kulishughulikia  suala la ujumi  wa Kiafrika,  Wafula  na Njogu
              (2007) wamebainisha misingi kadhaa ya ujumi huo. Baadhi ya misingi hiyo ni:


              (i)  Fasihi ya Kiafrika isifu Uafrika na kutilia mkazo utamaduni wa Kiafrika na
                   usawa wa watu wote.
              (ii)  Mashujaa wa Kiafrika na ushujaa wao vioneshwe katika kazi za kisanaa na
                   fasihi ya Kiafrika kwa jumla.

              (iii)  Lugha za Kiafrika zitumike katika uandishi wa fasihi ya Kiafrika.

              (iv)  Mbinu za utunzi  zifungamane  na mazingira  ya Kiafrika. Mbinu hizo
                   zihusishe  matumizi  ya vitu kama  vile  matumizi  ya mibuyu,  mikuyu,


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           117
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   117                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   117
   123   124   125   126   127   128   129   130   131   132   133