Page 124 - Fasihi_Kisw_F5
P. 124

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 4.16

              (a)  Kwa kutumia vyanzo vya mkondoni au vinginevyo, sikiliza wimbo wowote
                   wa bongo fleva kisha jibu maswali yafuatayo:
          FOR ONLINE READING ONLY
                   (i)  Chambua dhamira za wimbo huo.
                   (ii)  Je, ni athari  zipi  za kiimani na kimtazamo  zinazopatikana  katika
                        wimbo huo?

                   (iii)  Ni mitazamo gani inasawiriwa katika wimbo huo na ina athari zipi
                        katika jamii?
                   (iv)  Ni mitazamo ipi katika wimbo huo inasawiri au haisawiri jamii yako?

                   (v)  Una mtazamo upi wa jumla kuhusu wimbo huo?

              (b)  Chambua athari za kiimani na kimitazamo zilizomo katika mashairi mawili

                   ya diwani teule, kisha thibitisha namna zinavyojitokeza katika jamii.

              Athari za kiimani na kimtazamo katika tamthiliya zinavyojitokeza kwenye
              jamii
              Maudhui  ya tamthiliya  huwa na athari  za  kiimani  na za  kimtazamo  ambazo
              hujitokeza kwenye jamii husika. Maudhui hayo husambaa kupitia runinga, redio,
              na mitandao ya kijamii. Njia hizi zinarahisisha kusambaa kwa athari hizo na
              kuifikia hadhira kwa haraka.

               Shughuli ya 4.17

              (a)  Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.
                   Avita:    Nina wengine, siyo mwingine. Kwa uzuri huu wanaonitaka ni
                            wengi, lazima nibadili ladha.

                   Vera:    Hayo ndiyo maneno, unanipa raha best. Hahahaaaa!

                   Avita:     Tena siku hizi nina yule aliyekuwa wako ukamwacha ulipokwenda
                            chuo. Vipi na wewe huko chuoni umeshaopoa madaktari wangapi?

                   Vera:    Siyo madaktari tu, na maprofesa.

                   Avita:   Maprofesa? Sikuwezi. Unawapataje na madigrii yao vichwani?


                   Vera:    Uzuri best, uzuri, chema chajiuza.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           113
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   113                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   113
   119   120   121   122   123   124   125   126   127   128   129