Page 121 - Fasihi_Kisw_F5
P. 121

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (b)  Chambua mitazamo iliyomo kwenye mashairi mawili katika diwani teule,
                   kisha eleza namna inavyohusiana na matendo ya jamii.

              Uhusiano wa mitazamo iliyomo katika tamthiliya na matendo ya jamii
              Kama  ilivyo  kwa  bongo  fleva  na  mashairi,  tamthiliya  husawiri  mitazamo  na
          FOR ONLINE READING ONLY
              matendo ya wanajamii kama njia ya kujenga maudhui. Malengo ya maudhui hayo
              ni kuleta mabadiliko katika jamii kwa kuonesha matendo na mitazamo chanya
              kupitia wahusika wake. Hivyo, mazungumzo huwa ni malighafi ya msanii katika
              kusana kazi yake.
               Shughuli ya 4.14


              (a)  Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.
                   Bi Somoe:        Mata mwanangu, sisi wazazi wako ni masikini. Lakini
                                    hata siku moja hujasikia tumeiba mali ya ntu. Tusameheni
                                    wanetu  kwa kushindwa kuwasomesha. Ni sababu ya
                                    umasikini  wetu. Ingawa unajua  kusoma mawili  matatu.
                                    Lakini  huko njini  uendako kama kuna uwezakano wa
                                    kujiendeleza fanya hivyo. Kwani elimu haina mwisho.

                   Mata:            Sawa mama.

                   Bi Somoe:         Kila siku tunasikia kwenye maredio. Urithi wa ntoto ni
                                    elimu. Zamani tuliona heri watoto wetu tuwatumikishe tu
                                    kwenye mashamba ya mikorosho. Tulijua kuwa tungepata
                                    faida kubwa. Kumbe ulikuwa ni ujinga. Ungekuwa na elimu
                                    wala usingekwenda njini kwa mashaka. Ungekwenda njini
                                    kwa kazi yako.


                   Che Munndu:        Mama Mata unaongea  nini?  Wangapi wana elimu na
                                    wanaishi kwa mashaka?

                   Bi Somoe:         Kwani kuoa ni ujanja? Au kuoa wake wengi kila kukicha
                                    na kuwa na watoto wengi kama bata ndo ujanja?


                   Che Munndu:        Sasa hiyo unaona ni ujinga? Ndo maana kila mwananke
                                    ninayemwoa nampa talaka sababu ya ulozi wako.

                   Bi Somoe:         Nlozi we mwenyewe. Unaoa kila ukipata hela za
                                    korosho. Wanawake wanajua una pesa. Pesa zikikuishia
                                    wanakukimbia. Mbona mi  uliyenioa  na umaskini
                                    sikukimbii?


               110                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   110
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   110                   23/06/2024   17:54
   116   117   118   119   120   121   122   123   124   125   126