Page 116 - Fasihi_Kisw_F5
P. 116

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                         Nimejaliwa misitu natamka Tanzania,
                         Mngepata vingi vitu, siyo kama natania,

                         Lakini hamthubutu, wanyonge nasimulia,
          FOR ONLINE READING ONLY
                         Lakini Watanzania, mbona hamuendelei?



                         Kwa kweli nimemaizi, mama yenu Tanzania,

                         Pamoja na mali hizi, nyuma mnajirudia,
                         Wakiotesha mizizi, “weupe” mtajutia,

                         Lakini Watanzania, aliyewaroga nani?


                            Sibanduki (Hancha, 2015:16 - 17)

              (b)  Kwa kutumia  mashairi  mawili  kutoka  katika  diwani  teule,  chambua
                   mitazamo inayopatikana katika mashairi hayo.
              Mitazamo iliyomo katika tamthiliya
              Katika  kusawiri mambo  halisi  ya kijamii,  tamthiliya,  kama  tanzu  nyingine
              za fasihi andishi, hudhihirisha mitazamo  mbalimbali  iliyomo  katika  jamii.
              Mitazamo hiyo huwa na athari chanya au hasi katika jamii husika. Mitazamo
              chanya ikisawiriwa vyema katika tamthiliya, hadhira hujifunza na kupata maarifa
              mapya yanayowasaidia katika harakati zao za kuboresha maisha. Kinyume chake,
              mitazamo hasi hurudisha nyuma maendeleo ya kijamii.


               Shughuli ya 4.11
              (a)  Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.

                    Cheja:           (kwa hamaki) Juma! Huwezi kwenda namna hii hata kidogo.
                                   Huwezi kunikana na hali ulisema unanipenda. Nilikueleza
                                   siku ile hatari yake hukutaka  kunisikia.  Ukajisingizia
                                   mapenzi. Sasa leo unataka kunikana hivi. Hata kidogo!


                    Juma:            Hata kikubwa. Usinishikilie  hivyo.  Tena nakueleza  wazi
                                   usije ukalogwa kumwambia mtu kuwa mzigo huo ni wangu.
                                   Walahi utajuta.

                    Cheja:         Utafanya nini?





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           105
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   105                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   105
   111   112   113   114   115   116   117   118   119   120   121