Page 113 - Fasihi_Kisw_F5
P. 113

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Mtendaji kata:     Ondoka! Unaniwekea  kiwingu, nina kazi  nyingi  za
                                    kufanya.


                   Megno:           Nimekuja kuchukua fomu, nataka kugombea
          FOR ONLINE READING ONLY
                   Mtendaji kata:     Wala  usijisumbue  kunieleza,  ondoka.  Wewe ni kilema.
                                    Utamwongoza nani?

                   Megno:           Tafadhali mzee sikuja kudhalilishwa utu wangu.

                   Mtendaji kata:     Nimesema hakuna  fomu. (Akisema  kwa ukali) Ondoka
                                    nisikuone!

                   Megno:             Nashukuru sana mzee. (Megno anaondoka wakati mtendaji
                                    anaendelea kupekua mafaili yake).
                                           Changamoto (Mahenge, 2010: 5 - 6)


                   Maswali
                   (i)  Mhusika Mtendaji ana imani gani kuhusu Megno?

                   (ii)  Ni kwa namna gani maadili ya tamthiliya hii yanahusiana na imani za
                        jamii?
                   (iii)  Jamii inaamini nini kuhusu tukio la kumfukuza Megno?

                   (iv)  Una mtazamo gani juu ya mhusika Megno ukizingatia suala la imani
                        za jamii yako?

                   (v)  Mhusika Megno anaamini nini kuhusu hali yake?

              (b)  Chambua uhusiano uliopo kati ya maadili na imani katika tamthiliya mbili
                   teule.


              Mitazamo iliyomo katika bongo fleva, mashairi na tamthiliya
              Watunzi wa kazi za kifasihi husawiri mitazamo mbalimbali waliyonayo au
              iliyomo katika jamii. Hivyo, utunzi wa kazi zao huzingatia mitazamo hiyo na
              hukusudia kuishirikisha jamii. Mitazamo hiyo imeweza kujidhihirisha katika
              baadhi  ya  kazi  za  kifasihi  kama  vile  nyimbo  za  bongo  fleva, mashairi na
              tamthiliya.

              Mitazamo iliyomo katika bongo fleva
              Bongo fleva ni utanzu pendwa zaidi kwa watoto, vijalunga na watu wazima. Huu
              ni miongoni mwa tanzu zinazosambaa kwa haraka zaidi ikilinganishwa na tanzu
              nyingine za fasihi simulizi. Kutokana na hali hii, ni wazi kwamba mitazamo


               102                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   102
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   102                   23/06/2024   17:54
   108   109   110   111   112   113   114   115   116   117   118