Page 114 - Fasihi_Kisw_F5
P. 114

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              inayojitokeza katika nyimbo za bongo fleva husambaa haraka katika jamii kupitia
              majukwaa mbalimbali, yakiwamo yale ya mitandao ya kijamii. Ijapokuwa mingi
              ya mitazamo hiyo ni chanya, bado kuna baadhi ya nyimbo zenye mitazamo hasi
              inayosababisha zifungiwe na mamlaka husika.
          FOR ONLINE READING ONLY
               Shughuli ya 4.9
              (a)  Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni  na vinginevyo, sikiliza  wimbo wa

                   bongo  fleva  wa  msanii  yeyote  unaosawiri  athari  za  starehe,  kisha  jibu
                   maswali yafuatayo:

                  Maswali
                   (i)  Wimbo huo una dhamira zipi?

                   (ii)  Mtunzi ana mtazamo gani kuhusu starehe?
                   (iii)  Jamii  yako  ina  mitazamo  gani  kuhusiana  na  starehe  zinazofanywa
                        katika jamii?

                   (iv)  Mitazamo ya mtunzi wa wimbo huo inahusianaje na ile ya jamii yako?
                        Fafanua

                   (v)  Una mtazamo gani kuhusu wimbo huo?

              (b)  Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni au vinginevyo, sikiliza nyimbo mbili
                   za bongo fleva, kisha chambua mitazamo inayopatikana katika nyimbo hizo.

              Mitazamo iliyomo katika mashairi
              Watunzi wa mashairi ya Kiswahili wameibua mitazamo mbalimbali kupitia kazi
              zao. Baadhi ya mitazamo hiyo inasawiri maisha halisi, na inawataka wanajamii
              kubadilika ili kuwa na jamii yenye ustawi na uwajibikaji. Kupitia utanzu huu,
              wanajamii hujifunza kuhusiana na mitazamo iliyomo katika jamii.

               Shughuli ya 4.10

              (a)  Ghani au soma shairi lifuatalo, kisha chambua mitazamo iliyomo.

                         Natamka Tanzania
                         Nimejaliwa mabonde natamka Tanzania,

                         Kama Rufiji upande, wa Mashariki sikia,
                         Mazao mengi ja kunde, kumbe mngejilimia,

                         Lakini Watanzania, bado masikini mno.


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           103
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   103                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   103
   109   110   111   112   113   114   115   116   117   118   119