Page 118 - Fasihi_Kisw_F5
P. 118

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Maswali
                   (i)  Ni maudhui gani unayapata kupitia  mazungumzo  ya wahusika wa
                        matini hii?

                   (ii)  Wahusika wana mitazamo gani katika matini hii?
          FOR ONLINE READING ONLY
                   (iii)  Unapata mtazamo gani kuhusiana na Cheja anaposema “Sembuli
                        alinikosea kwa nguvu na sasa mimi ni mjamzito”
                   (iv)  Una maoni gani kuhusiana na matendo ya wahusika Cheja na Juma?
                        Je, yanapaswa kuigwa katika jamii? Kwa nini?

                   (v)  Mitazamo gani inajengwa na matukio ya mhusika Juma?

                   (vi)  Mbali na mitazamo iliyomo katika tamthiliya hii, una mitazamo gani
                        mingine kuhusiana na matini hii?

                   (vii) Unafikiri kuna uhusiano wowote kati ya mitazamo ya wahusika wa
                        tamthiliya hii na matendo ya jamii?

              (b)  Chambua mitazamo inayopatikana katika tamthiliya mbili teule ulizosoma.

              Uhusiano  wa  mitazamo  iliyomo  katika  bongo  fleva,  mashairi  na
              tamthiliya na matendo ya jamii
              Kuna uhusiano mkubwa kati ya kazi za kifasihi na matendo ya jamii  kwani
              watunzi hutunga kutokana na matendo yanayofanywa na wanajamii. Uhusiano
              wa mitazamo na imani ya jamii unaweza kuonekana katika baadhi ya kazi za
              kifashi kama vile nyimbo za bongo fleva, mashairi na tamthiliya.

              Uhusiano wa mitazamo iliyomo katika nyimbo za bongo fleva na matendo
              ya jamii
              Nyimbo za bongo fleva zimeonesha mitazamo mbalimbali inayosawiri matendo
              ya jamii. Kwa kupitia usawiri wa matendo hayo wasanii wamekuwa wakitoa
              mafunzo na maadili  kwa jamii  katika  maeneo  mbalimbali  ya maisha. Wakati
              matendo  hasi yana athari  mbaya kimaisha, matendo chanya yanaposawiriwa
              vyema,  wanajamii  hupata  maarifa  yanayowasaidia  kuleta  mabadiliko  chanya,
              hivyo kuchangia kwenye ustawi na maendeleo ya jamii.

               Shughuli ya 4.12

              (a)  Kwa kutumia vyanzo vya mkondoni au vinginevyo, sikiliza wimbo wowote
                   wa bongo fleva ulioimbwa na mtoto chini ya miaka kumi na minane (18),
                   kisha jibu maswali yafuatayo:


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           107
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   107                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   107
   113   114   115   116   117   118   119   120   121   122   123