Page 117 - Fasihi_Kisw_F5
P. 117

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                    Juma:            (Anacheka). Eti “utanifanya nini” kwanza utaniona wapi?
                                   Kwanza nani shahidi?

                    Cheja:          (kwa uchungu). Yaani kweli, Juma imekuwa si kitu kwako
                                   litakalonipata  baadaye.  Hunifikirii  nitamfanyaje  mtoto.
          FOR ONLINE READING ONLY
                                   (Anashindwa kusema kwa muda.) Kumbe yote  yalikuwa
                                   ulaghai mtupu. Siamini! Siamini!

                    Juma:            Amini! Amini tu! Wewe sikiliza. Jiendee zako kwa wazazi
                                   wako ukajitunze  kama  unaogopa  kuendelea  kukaa  kwa
                                   mwajiri wako. Nenda tu.

                    Cheja:           Sikuweza kuvumilia  kukaa tena nyumbani kwao.
                                   (Anatazama chini.) Hapana sikuweza.

                    Bw. Chowe:     Kwa nini?

                    Cheja:         (Kwa kusita hali akiwa bado anatazama chini.) Bwana Se
                                   … Bwana Sembuli alinikosea kwa nguvu na sasa mimi ni
                                   mjamzito…

                    Cheja:          Bwana Sembuli alinikosea  kwa nguvu na sasa mimi ni
                                   mjamzito. (Wote wanapigwa bumbuazi).

                    Bw. Chowe:   Eti nini? (Cheja anaanza kulia).


                    Bi. Chowe:       Uuuuuui, Uuuuuuuuuui Mungu wangu! (kwa wanawake
                                   wenzie)  Jamani  nielezeni  labda  sikusikia  vizuri.
                                   Uuuuuuuuuuuuui! (Anamkimbilia Cheja). Cheja mwanangu
                                   Uuuuuuuuuuui!

                    Bw. Chowe:    (kwa Bi. Chowe)  Aaa!  Acha kelele wewe. Sema vizuri
                                   Cheja sema acha kulia! Ati kweli au unatania?

                    Cheja:         Kweli baba.

                    Bi. Chowe:       Uuuuuuuuui! Uuuuuuuuuui! (Anakwenda kwa wanawake
                                   wenziwe). Uuuuuuui!

                                           Hatia (Muhando, 1974: 9-15).






               106                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   106
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   106                   23/06/2024   17:54
   112   113   114   115   116   117   118   119   120   121   122