Page 112 - Fasihi_Kisw_F5
P. 112

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                          Tumaini twaliweka, kwenu nafasi maisha,
                          Hatuna hata mkeka, sema utakuja kwisha,

                          Leo kumbe mwasikika, ipo siku mtakwisha,
          FOR ONLINE READING ONLY
                          Kwa nini mwatunyanyasa, wakati wote twaishi?


                            Kurunzi (Mbijima 2019: 33 - 34)

                   Maswali

                   (i)  Ni dhamira zipi za kimaadili zinazopatikana katika shairi hili?
                   (ii)  Ni maadili gani unayoyapata kutokana na shairi hili?

                   (iii)  Ni imani zipi unazozipata kutoka katika shairi hili?

                   (iv)  Kuna uhusiano gani kati ya maadili yaliyoelezwa katika shairi hili na
                        maadili ya jamii yako?

                   (v)  Ni kwa namna gani maudhui ya shairi hili hayaendani na maadili ya
                        jamii yako?

              (b)  Chagua mashairi mawili kutoka katika diwani mbili teule, kisha husianisha
                   maadili yaliyomo na imani za jamii.
              Ulinganisho wa maadili na imani katika tamthiliya
              Tamthiliya husawiri mambo halisi yanayotokea katika jamii, aghalabu utanzu
              huu umeweza kuonesha uhusiano uliopo kati ya maadili na imani za jamii husika.
              Kupitia utanzu huu, wanajamii huweza kujifunza namna ya kuishi na watu wa
              hali mbalimbali kwa kuzingatia misingi ya kiimani na kimaadili.

               Shughuli ya 4.8

              (a)  Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.
                   Megno:           Habari za asubuhi Mtendaji

                   Mtendaji kata:   (Kwa hasira) hatutoi misaada hapa, ondoka!


                   Megno:           Aliyekwambia nimekuja kuomba msaada ni nani?

                   Mtendaji kata:    Kilichokuleta nini?

                   Megno:           Msidharau watu jamani. Hatukupenda kuwa hivi.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                           101
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   101                   23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   101
   107   108   109   110   111   112   113   114   115   116   117