Page 107 - Fasihi_Kisw_F5
P. 107

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 4.4

              (a)  Soma matini fupi ya tamthiliya ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.
                   Huka:            (anaanza kulia.)
          FOR ONLINE READING ONLY
                   Ngahinyana:      Eeh! Ukweli unauma sasa...

                   Mama Huka:         Aaa, Baba Huka, usimfikirie mtoto mambo mabaya.

                   Ngahinyana:        Hapana. Huyu mtoto  amekwishaanza kuharibika.  Mara
                                    nyingi, nimeandikiwa  barua na babake mdogo kusema
                                    Huka hatulii,  na wewe hukuamini ukasema wanaanza
                                    kumsingizia  mtoto  wako,  mpaka  tukagombana  na
                                    aliyekuwa akitusomea barua zetu. (Mara hodi inasikika).
                                    Ehee! Sasa utaniona; nitamnyosha barabara.  (Anachukua
                                    fimbo yake iliyokuwa ikiegemea ukutani na anakwenda
                                    karibu na mlango na anainua fimbo kungojea ishuke mara
                                    tu apigaye hodi atakapoingia.) Karibu. Fungua mlango.


                   Mama Huka:        Hapana baba Huka! (Anamshika lakini anasukumwa). Si
                                    vizuri.

                   Ngahinyana:       Sogea huko! (Mgeni anaingia na fimbo ya mzee inashuka
                                    na kutua begani mwake). Wewe ndiye ...

                   Pata:              (Anaanguka kwa uchungu na barua alizozishika
                                    zinatapakaa chini.) Ochchchch! Mzee vipi? Nimekukosea
                                    nini?  Ahaa  (Anainuka  na kushika bega lake.  Ndipo
                                    Ngahinyana  anapogundua  kosa  lake.  Huka  baada  ya
                                    kuona barua anatoka).


                   Ngahinyana:       Oh! Pole  sana  mwanangu,  sikujua  kama  ni  wewe.
                                    Tulikuwa  tunamtegemea  mpumbavu  mmoja.  Lakini
                                    bahati  yake. Pole sana mwanangu! (Anasaidia kuokota
                                    barua).

                   Pata:              Loo! Pameuma. Pole tu haisaidii kitu. Mzee siku nyingine
                                    uwe na uhakika  au la  tutaogopa  kukuletea  barua  zako.
                                    Unaonesha kuwa ni mkali sana!



                96                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   96                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   96
   102   103   104   105   106   107   108   109   110   111   112