Page 103 - Fasihi_Kisw_F5
P. 103

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              maamuzi,  tabia  na  uhusiano  wa watu  katika  maisha  ya  kila  siku.  Baadhi  ya
              watunzi  na  waandishi  wa kazi  za  sanaa  huyapa  kipaumbele  maadili  katika
              kazi zao. Kutokuzingatia misingi ya maadili katika utunzi wa kazi za kifasihi
              huchangia kumomonyoka kwa maadili katika jamii. Hivyo basi, misingi hiyo
          FOR ONLINE READING ONLY
              inapaswa kuzingatiwa katika utunzi wa kazi mbalimbali za kifasihi, zikiwamo
              nyimbo za bongo fleva mashairi na tamthiliya.

              Misingi ya maadili katika jamii
              Misingi ya maadili huweza kutofautiana baina ya jamii moja na nyingine. Hata
              hivyo, kuna misingi ya jumla ambayo hutawala katika jamii mbalimbali. Baadhi
              ya mifano ya misingi hiyo ni heshima, utii, haki na usawa, uwajibikaji, uaminifu
              na uwazi:

                   (i)  Heshima:  ni hali  ya kujithamini  na kuwathamini  wengine, mali  na
                        mazingira yao. Heshima huweza kujengwa kwa ukarimu, uvumilivu,
                        uelewa  na  kuthaminiana  miongoni  mwa  watu.  Aidha,  heshima
                        hudumisha umoja, amani, maelewano,  nidhamu na maendeleo  ya
                        jamii.

                   (ii)  Utii: kipengele cha maadili ambacho  huhusiana na nidhamu na
                        kukubali maagizo au majukumu ambayo mtu hupewa, aghalabu  na
                        mtu aliye juu yake kiumri au kimamlaka. Pia, utii huendana na kuafiki
                        au kutekeleza sheria au miongozo ya kijamii. Msingi huu wa uadilifu
                        huleta maendeleo katika jamii na huchochea kuwapo kwa umoja na
                        ushirikiano.

                   (iii)  Haki na usawa: katika jamii yenye haki na usawa, watu wanapaswa
                        kuwa salama, wenye uhuru kamili, na wasio na hofu ya kudhulumiwa
                        wala kutengwa. Haki na usawa hulinda watu dhidi ya ubaguzi wowote,
                        kwa misingi ya rangi, jinsi, dini, au utaifa. Kila mmoja ana thamani
                        na  mchango  katika  kuleta maendeleo  ya  jamii  yake.  Hivyo, jamii
                        inayotambua haki na usawa hutoa elimu bora, huduma za afya na fursa
                        za kiuchumi kwa usawa ili kujenga maisha bora kwa mtu mmojammoja
                        na wanaomzunguka.
                   (iv)  Uwajibikaji: unahusu kutimiza majukumu kikamilifu na kwa wakati.
                        Kila  mtu  anapaswa  kutekeleza  majukumu  yake  ili  kuleta  tija  na
                        maendeleo katika jamii.






                92                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   92
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   92                    23/06/2024   17:54
   98   99   100   101   102   103   104   105   106   107   108