Page 104 - Fasihi_Kisw_F5
P. 104
Fasihi ya Kiswahili kwa Shule za Sekondari
(v) Uaminifu ni hali ya mtu kuwa mnyoofu mwenye tabia njema
inayosababisha akubalike na watu na jamii inayomzunguka. Uaminifu
huzingatia msimamo alionao mtu bila kuathiriwa na ushawishi wa
mtu mwingine. Uaminifu hujenga imani na heshima. Pia, huimarisha
FOR ONLINE READING ONLY
uhusiano mwema kuanzia ngazi ya familia na maeneo mengine kama
vile kazini, kwenye nyumba za ibada, na kwenye asasi na taasisi
mbalimbali.
(vi) Uwazi: unahusu fursa ya kila mwanajamii kujua mambo ya
kimaendeleo yanayotokea au kufanyika katika jamii yake. Uwazi
pia hutakiwa kudhihirishwa na kila mmoja kuanzia katika ngazi ya
familia.
Umuhimu wa maadili katika jamii
Maadili hujenga amani na utulivu na huleta umoja, ushirikiano na kuheshimiana
miongoni mwa wanajamii. Hali hii huondoa vitendo vya ukatili na uonevu
ambavyo huweza kusababisha migogoro au machafuko katika jamii.
Zaidi ya kuleta maendeleo katika jamii, maadili huwafanya watu wawe wawazi,
wakweli, na waaminifu katika kutunza mali au rasilimali za umma. Mathalani,
viongozi waadilifu huweza kuchangia maendeleo kwa kusimamia vizuri
rasilimaliwatu na rasilimalifedha zilizoko katika maeneo yao ya kazi. Vilevile,
maadili hujenga uzalendo na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya maendeleo
binafsi na ya jamii kwa ujumla. Maadili huwafanya watu watambue umuhimu
wa kushiriki katika miradi ya kijamii na kuchangia katika maendeleo ya sekta
mbalimbali kama vile elimu na afya. Zaidi ya hayo, maadili hupunguza ufisadi,
uhalifu na migogoro katika jamii. Kwa hiyo, maadili huchangia katika kuboresha
maisha ya watu na kujenga ustawi. Umuhimu wa maadili umeweza kudhihirika
katika kazi za fasihi kama vile bongo fleva, mashairi na tamthiliya kama
inavyofafanuliwa hapa chini:
Maadili katika nyimbo za bongo fleva
Nyimbo za bongo fleva zilianza kuimbwa kuanzia miaka ya 1990 hadi sasa na
zimekuwa zikiimbwa na kupendwa sana na watu ndani na nje ya bara la Afrika.
Nyimbo hizi zimekuwa zikiwavutia watu kwa sababu mbalimbali kama vile
mahadhi yake na matumizi ya lugha ya kisanaa. Baadhi ya nyimbo zimetumia
lugha ya picha katika kufikisha ujumbe kwa jamii. Mbali na kutumia lugha
ya kisanaa, nyimbo hizi zimekuwa zikielimisha na kuburudisha kwa namna
mbalimbali. Licha ya baadhi ya nyimbo hizi kukiuka misingi ya kimaadili
kutokana na kutumia lugha zisizo na staha. Hata hivyo, nyingine zimekuwa
zikizingatia maadili yanayofundisha na kujenga jamii.
Kitabu cha Mwanafunzi 93
Kidato cha Tano
23/06/2024 17:54
FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd 93 23/06/2024 17:54
FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd 93