Page 99 - Fasihi_Kisw_F5
P. 99

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Kutokana na kufanya shughuli ulizopewa, na kujibu maswali uliyoulizwa, utakuwa
              umejifunza namna ya kuzitumia nadharia za umaksi na mwingilianomatini katika
              kuhakiki kazi za fasihi.


               Shughuli ya 3.17
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kwa kutumia kazi za ushairi au tamthiliya teule, eleza mchango wa nadharia ya
              mwingilianomatini katika maendeleo na uhakiki wa tanzu hizo.


              Kutathmini mchango wa nadharia teule za uhakiki wa kazi za fasihi
              katika maendeleo ya ushairi na tamthiliya
              Kila utanzu wa fasihi hupitia mabadiliko yanayotokana na sababu mbalimbali.
              Sababu hizo huweza kuwa za kijamii, kisiasa, kiutamaduni, kiuchumi, na
              kitaaluma. Yote haya huathiri pia maendeleo na kukua kwa taaluma ya uhakiki
              ambapo wahakiki huwa na wigo mpana wa kuibua na kutumia nadharia
              mbalimbali za kihakiki. Mathalani, katika utanzu wa ushairi mabadiliko
              yaliyotokea hadi kuibua mvutano baina ya washairi wa kijadi/kimapokeo na
              wa kisasa ulichangia katika kuibua mawazo na aina mpya ya ushairi. Kutokana
              na hali hii maana ya ushairi wa Kiswahili ilibadilika. Halikadhalika, utanzu
              wa tamthiliya ulipitia mabadiliko yaliyotokana na udadisi na ubunifu wa
              wanatamthiliya na wahakiki waliosaili utunzi unaofuata kanuni za Kiaristotle.
              Utanzu wa tamthiliya za Kiswahili ukaanza kutumia kanuni za kijadi za fasihi
              simulizi, sanaa za maonesho za Kiafrika, pamoja na kuakisi mazingira ya
              Kiafrika. Mchakato huo uliibua tamthiliya za Kiswahili zenye ladha ya Kiafrika.

              Mabadiliko na maendeleo ya tanzu za ushairi na tamthiliya yaliathiri na kuibua
              nadharia mbalimbali za uhakiki zilizochangia maendeleo ya tanzu hizi. Nadharia
              hizi  zimeendelea  kutumika  kama  mwongozo  wa jumla  katika  kujenga  hoja
              wakati wa kuhakiki kazi mbalimbali za fasihi. Vilevile, nadharia hizi humsaidia
              mhakiki kuibua na kuchochea udadisi katika kubaini changamoto mbalimbali
              zinazoikabili  jamii.  Halikadhalika,  nadharia  humsaidia  mhakiki  kuchunguza
              na kuifahamu jamii katika nyanja mbalimbali, kama vile za kiuchumi, kisiasa,
              kiutamaduni  na kijamii. Aidha, nadharia humsaidia mhakiki kujenga hoja na
              kumwezesha kuweka bayana changamoto au matatizo yanayoikumba jamii. Pia,
              humwezesha mhakiki kugundua au kuboresha jambo jipya. Kwa msingi huo,
              nadharia ni muhimu sana katika maendeleo ya kazi mbalimbali za fasihi.










                88                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   88
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   88                    23/06/2024   17:54
   94   95   96   97   98   99   100   101   102   103   104