Page 96 - Fasihi_Kisw_F5
P. 96

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                  Basi baba yako katuachia  kichwa cha tembo.  Tumewinda
                                pamoja.  Jamaa zake amewapa meno na usinga. Na sisi
                                ametuachia kichwa cha tembo. Sasa naelewa kwa nini hakutia
                                saini  hati.  Mwenyekiti  sasa hivi  anatayarisha  mazishi  ya
          FOR ONLINE READING ONLY
                                Herbert.
                                  Anataka kumzika Herbert Kikiristo. Hiyo ni dhima yetu. Ni
                                dhima yangu. Anataka kumzika Herbert na kuandikisha kila
                                kitu katika jina la Umma Klan.

                                Kila kitu. Nyumba, viwanja, gari, fanicha kila kitu.

                                  Unavyotuona hapa,  sisi ni  maskini.  Ndiyo  maisha  ya
                                mwanamke. Unapoteza mume. Unapoteza maisha. Unapoteza
                                kila kitu.
                                (Kimya)

                                  Na wewe unafanya nini? Unalialia tu hapa. Utaniona mimi
                                kulia? Unaniona mimi kujiuliza maswali ya kijinga? Hapana!
                                Kwa sababu najuwa mimi nani? Na wajibu wangu ni nini?
                                (Kimya)


                                  Kweli, kuna wakati hata mimi natamani ningekuwa maiti,
                                simo katika maisha, nikaepukana na ujinga huu.
                                (Anabadilisha sauti. Anakumbuka)

                                  Ingekuwa uzuri ningekufa siku ile nilipokuwa msituni. Ilikuwa
                                siku za Mau Mau. Nilikuwa naumwa malaria kali sana. Scouts
                                walikuwa  wanatutafuta.  Walipata  habari  wapi  tumejificha.
                                Wenzangu  wote  walikimbia.  Wapiganaji  wawili,  Njiru  na
                                mwenziwe, walipigwa risasi wakafa palepale msituni. Mimi
                                nikajikokota. Nikajificha kwenye kichaka, kwenye majani.

                                  Scouts wakaja  mpaka  pale  nilipokuwa.  Ajabu!  Sikuogopa.
                                Nilikuwa tayari mimi kufa.
                                (Kimya)

                                  Ingekuwa uzuri ningekufa! Ningekufa peke yangu kuliko hivi.
                                Watu chungu nzima! Rafiki tele! Bure tu. Jamaa zangu damu
                                moja. Wamenitenga siku ya ndoa.



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            85
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   85                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   85
   91   92   93   94   95   96   97   98   99   100   101