Page 95 - Fasihi_Kisw_F5
P. 95

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Chris:           Ma! Mimi nani?

                   Martha:          Wewe? (Kimya) Wewe Chris.

                   Chris:             Chris! Chris! (Ana uchungu) Haunielewi. Na maana:
          FOR ONLINE READING ONLY
                                    Mimi hasa ni nani? Bado haujaelewa.

                   Martha:            Naelewa.  Unatoka kusikiliza  maneno ya wahuni
                                    barabarani.
                                    (Baada ya muda)

                                    Mimi Martha. Wewe Chris.

                   Chris:             Kila  ukiniandikia  barua,  ukizungumza  kwenye  simu,
                                    unanieleza habari ya familia. Iko wapi familia? Mbona…

                   Martha:          Sitaki maneno hayo.

                                    (Kimya)

                   Chris:           (Anasikitika)

                                    Baba, maskini, baba!

                   Martha:           Mwisho… Jambo la mwisho kabisa baba yako angependa
                                    kusikia… ni huku kuomboleza, kuomboleza.

                   Chris:           Baba yangu? Kwani kweli baba yangu?

                                    (Kibao)

                   Martha:        Sijui huko  Amerika wanafundisha nini? Ukitoka nje,
                                ukirudi  mara hili.  Sasa hujui  mimi  nani,  wewe nani?
                                Umechanganyikiwa. Unalialia na kupenga makamasi tu hapa.
                                Lakini utakua kweli wewe, ukawa mtu hasa wa kukutegemea?
                                Baba zima.  Litazame.  Utaweza kushika madaraka  ya aina
                                yoyote wewe? Utaweza kusimama mahali pa baba yako?

                   Chris:         Kushika mahali  pa baba?  Nani atanisikiliza?  Nitaanzaje?
                                Huku siko… siko kokote!
                                (Analia)

                   Martha:        Msikilize, hana hata haya. Unajua maana ya kuachiwa kichwa
                                cha tembo? Haujui.


                84                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   84
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   84                    23/06/2024   17:54
   90   91   92   93   94   95   96   97   98   99   100