Page 94 - Fasihi_Kisw_F5
P. 94

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                Mume
                                Aaa! nimetambua, tumtafute Uledi,

                                Ili apike chakula, afue nguo nyumbani,
          FOR ONLINE READING ONLY
                                Akitandike kitanda, adeki na sebule,
                                Haya maisha ya ndoa, wenzangu mnaishije?
                                Nguo zetu kunyoosha, anifunge yangu tai,

                                Viatu vyako kuvaa, afunge yangu lesani,
                                Mke wangu pumzika, kwa uchovu wa kazini

                                Haya maisha ya ndoa, wenzangu mnaishije?



                                    Kurunzi (Mbijima, 2019: 17 – 20)

                   (i)  Shairi hili lina nafasi gani katika kuleta usawa wa kijinsia katika jamii?

                   (ii)  Mshororo usemao “mke msomi ni shida, wanaume tuna kazi” unaibua
                        hisia gani?
                   (iii)  Ni kwa namna gani shairi hili linaipambanua  hali ya mwanamke
                        kiuyakinifu?

                   (iv)  Jadili uumbaji wa wahusika katika shairi hilo?

                   (v)  Ni kwa namna gani shairi hili linaakisi maisha halisi ya jamii?

              (c)  Hakiki mashairi mawili kutoka katika diwani teule kwa kutumia nadharia

                   ya ufeministi.
              Kutokana na kufanya shughuli ulizopewa, na kujibu maswali uliyoulizwa,
              utakuwa umejifunza namna ya kuzitumia nadharia za umuundo na ufeministi
              katika kuhakiki kazi za fasihi.

               Shughuli ya 3.16

              (a)  Hakiki kipande cha tamthiliya kifuatacho kwa kutumia nadharia ya umaksi
                   ukiongozwa na maswali yanayofuata.
                   (Mahali ni palepale  kama kwenye  onesho la kwanza. Mapambo
                   yameondolewa. Martha amekaa kwenye kiti cha marehemu. Chris ameweka
                   kichwa  chake  katika  mikono yake. Martha anajishughulisha kuandaa
                   chakula cha mchana)


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            83
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   83                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   83
   89   90   91   92   93   94   95   96   97   98   99