Page 90 - Fasihi_Kisw_F5
P. 90

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (b)  Tazama  maigizo  katika  runinga au vifaa  vingine  vya  TEHAMA, kisha
                   chambua maigizo matatu kwa kutumia nadharia ya mwitiko wa msomaji,
                   huku ukiongozwa na maswali yafuatayo:

                   (i)  Ni maana zipi zinaweza kupatikana katika maigizo hayo?
          FOR ONLINE READING ONLY
                   (ii)  Kwa maoni yako, ni miktadha gani imetumika  katika  utunzi wa
                        maigizo hayo?

                   (iii)  Je, msomaji anaweza kupata athari zipi kutokana na maigizo hayo?

                   (iv)  Maigizo hayo yana uhusiano gani na mazingira yako?
                   (v)  Una maoni gani kuhusu usahihi wa maigizo hayo?

              Kutokana na kufanya shughuli ulizopewa, na kujibu maswali uliyoulizwa,
              utakuwa umejifunza namna ya kuzitumia nadharia za uhalisia na mwitiko wa
              msomaji katika kuhakiki kazi za fasihi.

              Kuhakiki mashairi kwa kutumia nadharia za kifasihi

               Shughuli ya 3.14
              Soma na hakiki shairi lifuatalo kwa kutumia nadharia ya umuundo.


                       Hutaniacha Morogoro

                       1.  Ninapotazama saa, ni saa saba mchana,
                           Watu wengi wamekaa, stendi wasukumana,
                           Nasikia “Daa! Daa! Basi lenu mwaliona!”

                           Kondakta kwa kupaaa, sauti hiyo anena,
                           Ndipo ninapoutwaa, mfuko naingizana,

                           John ananiambia, “hutan’acha Morogoro!”


                       2.  Niingiapo basini, kuna mtu anikuna,
                           Anipapasa begani, kama vile twajuana,
                           Najifanya simuoni, pilika zimenibana,

                           Ghafula aja usoni, namwona ana kwa ana,
                           Kumbe ni kijana John, ni mwanangu wa ujana,

                           John ananiambia, “hutan’acha Morogoro!”




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            79
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   79                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   79
   85   86   87   88   89   90   91   92   93   94   95