Page 88 - Fasihi_Kisw_F5
P. 88

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kazi ya sanaa ili kubainisha maadili, ujumbe, msimamo na falsafa ya kazi hiyo
              kwa wanajamii. Kwa mujibu wa mtazamo huu, mhakiki ni mwalimu wa jamii
              kwa kuwa humfundisha msomaji kuhusu yale yaliyomo katika kazi ya fasihi.
              Aidha, mhakiki  humweleza mwandishi  kuhusu mambo  yaliyomo  katika  kazi
          FOR ONLINE READING ONLY
              yake ambayo yanakubalika au hayakubaliki kwa jamii (Senkoro, 1973).

              Mtazamo wa pili haumchukulii mhakiki kama mtu muhimu katika fasihi. Hii ni
              kwa sababu, mwandishi ndiye mhakiki mwenyewe. Hivyo, huweza kujikosoa na
              kurekebisha kazi yake mpaka anaporidhika nayo. Mtazamo huu pia huona kuwa
              mhakiki anajipachika vyeo ambavyo hastahili kwa kusema kuwa ni mwalimu
              wa msanii na msomaji  kwa sababu wasomaji wa kazi za fasihi wana uwezo
              wa kusoma na kuelewa; na hawahitaji watu wa kuwafafanulia. Kila msomaji
              anaaminika  kuwa na uwezo wa kuchambua kazi inayohusika; uchambuzi
              hutofautiana kutoka mtu mmoja hadi mwingine. Kwa mantiki hiyo, haitakiwi
              kumtegemea mhakiki ambaye naye ana mawazo yake kulingana na uwezo wake
              wa kuchambua na kufafanua kazi inayohusika (Mbele, 1993).


              Kwa mtazamo wa kwanza, mhakiki wa kazi za fasihi ana dhima zifuatazo:
              (i)  Kuchambua kila kipengele cha fani na maudhui.

              (ii)  Kubainisha dhamira zinazotolewa katika kazi za fasihi.

              (iii)  Kuhimiza na kushirikisha fikra za kihakiki kwa wanataaluma wengine.
              (iv)  Kukuza kiwango cha usomaji wa kazi za fasihi.

              (v)  Kumwelekeza msomaji ili apate maarifa zaidi.

              (vi)  Kufafanua nadharia zilizotumika katika kuhakiki kazi husika.
              (vii) Kubainisha misingi bora ya uandishi wa kazi za fasihi.

              (viii) Kuonesha uzuri na upungufu wa kazi iliyohakikiwa kwa lengo la kuelimisha
                   jamii na waandishi wa kazi za fasihi.


                                Zoezi la 3.2



                 1.   Eleza tofauti kati ya nadharia na nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi.

                 2.   Jadili kwa kutumia mifano umuhimu wa nadharia za uhakiki wa kazi za
                     fasihi.





                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            77
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   77                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   77
   83   84   85   86   87   88   89   90   91   92   93