Page 85 - Fasihi_Kisw_F5
P. 85

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 3.10
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, fafanua maana na misingi ya

              nadharia ya mwitiko wa msomaji katika kuhakiki kazi za fasihi.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Nadharia ya mwitiko wa msomaji
              Nadharia ya mwitiko wa msomaji huhusu namna msomaji  anavyoikabili,
              anavyoifasili na kuipa kazi ya fasihi maana kutokana na tajriba yake.


              Mmoja  wa  waasisi  wa  nadharia  hii  ni  Wolfgang  Iser  (1926  -  2007)  ambaye
              anajulikana kama baba wa nadharia hii.


              Kwa kawaida, mwandishi anapoandika kazi yake hutawaliwa na mambo kama
              vile  mazingira,  historia  au muktadha  wa jamii  yake.  Kwa upande  mwingine,
              msomaji wa matini naye huathiriwa na mambo kama vile uelewa binafsi, aina
              ya matini  anayosoma,  utamaduni,  mtindo  wa usomaji,  uzoefu wake juu ya
              jambo analolisoma, mazingira, historia, na matarajio yake. Mambo haya ndiyo
              husababisha  tofauti  ya  uelewekaji  wa matini  baina  ya  msomaji  mmoja  na
              mwingine. Kwa hiyo basi, nadharia hii huhusisha mambo matatu: mtunzi wa
              kazi ya fasihi, kazi husika ya fasihi, na hadhira. Pia, husisitiza kuwa hadhira
              hukamilisha maana kwa sababu msomaji ndiye anayelengwa na mwandishi; pia
              maana ya matini inategemea namna msomaji atakavyoelewa.

              Misingi ya nadharia ya mwitiko wa msomaji
              Ifuatayo ni misingi ya nadharia ya mwitiko wa msomaji:

              (i)  kazi ya fasihi haina maana moja;

              (ii)  maana ya kazi ya fasihi hukamilishwa na miktadha mbalimbali inayotokana
                   na tajriba ya msomaji;

              (iii)  mchakato wa usomaji na uelewaji wa kazi ya fasihi huhusisha matarajio ya
                   msomaji; na
              (iv)  tofauti za kitamaduni, kielimu, kisiasa, na kiuchumi husababisha tofauti za
                   maana ya kazi ya fasihi kati ya msomaji mmoja na mwingine.

              Unapohakiki  kazi  ya  fasihi  kwa kutumia  nadharia  ya  mwitiko  wa msomaji
              unatakiwa kuzingatia misingi iliyobainishwa.









                74                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   74                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   74
   80   81   82   83   84   85   86   87   88   89   90