Page 82 - Fasihi_Kisw_F5
P. 82

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   (iii)  watunzi wa kazi za fasihi kuwa na jukumu la kufichua, kudadisi na
                        kukosoa mifumo ya kibwanyenye;

                   (iv)  kuwapo kwa kupigania haki za mtu/jamii; na
                   (v)  kubainisha vipengele kama vile maadili, itikadi, dini na utamaduni na
          FOR ONLINE READING ONLY
                        namna vinavyoathiri maisha ya jamii.

              Unapochambua  kazi ya kifasihi kwa kutumia  nadharia  ya umaksi, unatakiwa
              kuchunguza namna mwandishi anavyoibua harakati za kitabaka katika kazi hiyo,
              mifumo ya uzalishaji mali, namna kazi hiyo inavyodadisi mambo mbalimbali
              katika jamii, na kupigania haki za mtu/jamii. Pia, unatakiwa kuhakiki vipengele
              mbalimbali  vya maisha (maadili,  itikadi,  dini na utamaduni),  migongano ya
              kijamii, na muundo wa jamii kwa kuangalia hali ya uchumi wao. Zaidi, unatakiwa
              kubainisha msimamo wa mwandishi wa kazi hiyo katika kuleta mabadiliko kwa
              jamii. Iwapo unachambua tamthiliya kama vile Kwenye Ukingo wa Thim (Hussein
              1988),  Nguzo  Mama  (Muhando 1982),  Kivuli  Kinaishi  (Mohamed 1990), na
              Ngoma ya Ng’wanamalundi (Mbogo 1988), zingatia namna vipengele kama vile
              migogoro ya kitabaka inavyosawiriwa hadi kupatikana kwa haki ya wanyonge.

               Shughuli ya 3.8
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, fafanua maana na misingi ya
              nadharia ya ufeministi katika kuhakiki kazi za fasihi.

              Nadharia ya ufeministi
              Ufeministi ni nadharia iliyojikita kwenye harakati za kupigania ukombozi wa
              mwanamke dhidi ya mifumo kandamizi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Mifumo
              hii imelenga kumkandamiza, kumnyonya na kumbagua mwanamke. Lengo la
              nadharia ya ufeministi ni kubainisha vipengele vya mifumo hii ili kupata suluhu
              ya matatizo yanayomkabili mwanamke katika hali mbalimbali.


              Baadhi ya waasisi wa nadharia hii ni Mary Wollstonecraft (1759 - 1797), Virginia
              Woolf (1882 - 1941) na Simeon de Beauvoir (1908 - 1986). Awali ufeminisiti
              uliibuka kama vuguvugu la kisiasa, ambapo lengo lake lilikuwa kuwainua
              wanawake kutoka katika hali ya kukandamizwa, kunyanyaswa, na kutengwa;
              na hivyo, kuwawezesha kupata haki ya kujieleza. Wanafeministi wa mwanzo
              walizungumzia matatizo yao kwa njia ya maandishi au machapisho na wakati
              mwingine mihadhara. Walikosoa na kuzipiga vita asasi kama vile za dini, ndoa
              na utamaduni zinazomdhalilisha au kumdunisha mwanamke.






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            71
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   71                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   71
   77   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87