Page 78 - Fasihi_Kisw_F5
P. 78

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (a)  Kuwavutia wasomaji
              Kazi  iliyopambwa kwa sanaa  huwavutia  wasomaji  kutamani  kuisoma  na
              kuielewa.  Wasomaji  hupenda kazi  za fasihi ambazo huwafanya wasichoke
              kusoma na wauishi ulimwengu wa kazi hiyo. Kwa mfano, kutumia mbinu nzuri
          FOR ONLINE READING ONLY
              za kisanaa huwezesha kufikisha ujumbe husika, kuielewa na kuifurahia kazi ya
              fasihi.

              (b)  Kuchochea mawazo na hisia kwa wasomaji
              Uandishi wenye mifano ya kina na uumbaji wa wahusika na mandhari kiubunifu
              huwafanya  wasomaji  kuhisi  na  kufikiri  zaidi.  Kazi  za  fasihi  zinazochochea
              mawazo na kuibua hisia husaidia kuleta mabadiliko ya kifikra, kuongeza ubunifu
              na maarifa,  na kuwapa wasomaji mtazamo  tofauti kuhusu maisha na duniani
              wanamoishi.

              (c)  Kuipa maana kazi ya fasihi
              Wasomaji wengi hupenda kufuatilia hadithi au tukio fulani na hutamani kulijua
              zaidi, yamkini kutokana na mafunzo ama ujumbe uliomo ndani yake. Maudhui
              yaliyomo ndani ya kazi ya fasihi huwafanya wasomaji kuutazama ulimwengu
              kwa  jicho  la  tofauti  na  kuwafikirisha  kuhusu  masuala  muhimu  katika  jamii.
              Hivyo, maudhui husaidia kubaini mafunzo yatokanayo na kazi za fasihi.


              (d)  Kuongeza ubora na upekee wa kazi ya fasihi
              Mwandishi anayetumia  ubunifu mkubwa uliojaa  mbinu  za kifasihi  katika
              mtindo wake wa uandishi huongeza ubora wa kazi na kutofautisha kazi hiyo na
              nyingine. Matumizi ya tamathali za semi na taswira mbalimbali husaidia kuumba
              ulimwengu mbadala ambao unaakisi ukweli na uongo, hali ambayo huzidisha
              ubunifu wa kazi za fasihi.

              (e)  Kukuza stadi za uandishi wa kazi za fasihi
              Ufahamu wa kina  wa vipengele  vya fani na maudhui  huwasaidia  waandishi
              kuandika kwa umahiri mkubwa.


                                Zoezi la 3.1



                 1.   “Fani na maudhui havina umuhimu katika kazi za fasihi”. Jadili hoja hii
                     kwa mifano thabiti kutoka katika kazi teule za fasihi.

                 2.   Fafanua kauli kwamba “uhusiano wa fani na maudhuii ni kama chai na
                     kikombe”.



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            67
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   67                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   67
   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83