Page 75 - Fasihi_Kisw_F5
P. 75

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari






                    Sura

                      ya                 Kutathmini kazi za fasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
                     Tatu







                          Utangulizi

               Kutathmini kazi za fasihi ni muhimu kwa sababu kunajenga uwezo wa kiakili na
               kihisia, kukuza stadi za uchambuzi na uandishi, kuchochea mawazo na kuelewa
               muktadha wa kihistoria  na kijamii.  Katika  sura hii  utajifunza,  mitazamo,
               uhusiano na dhima ya vipengele vya fani na maudhui katika kazi za fasihi. Pia,
               utajifunza nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi pamoja na kuzitumia katika
               kuchambua kazi mbalimbali za kifasihi. Umahiri utakaoujenga katika sura hii

               utakuwezesha kukuza stadi za uchambuzi na uandishi wa kazi za kifasihi.





                            Fani bila maudhui



               Shughuli ya 3.1

              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni au maktabani na vinginevyo, soma matini
              zinazohusu mitazamo mbalimbali ya dhana za fani na maudhui.


              Mitazamo kuhusu fani na maudhui
              Kuna mitazamo miwili inayoeleza  fani na maudhui nayo ni: mtazamo  wa
              kidhanifu na wa kiyakinifu. Sehemu inayofuata inafafanua mitazamo hiyo.


              Mtazamo wa Kidhanifu
              Mtazamo wa kidhanifu ni ule unaochukulia fani na maudhui kama vipengele
              ambavyo havina uhusiano, yaani kila kimoja kinajitegemea. Kwa mtazamo huu,
              katika kazi za fasihi, fani na maudhui huweza kutenganishwa na kila kimoja
              kikajitegemea.  Hivyo,  mtunzi  anaweza  kufikisha  ujumbe  wake  kwa  hadhira
              aliyokusudia bila kutilia maanani fani. Sengo na Kiango (1973) na Nkwera (1978)
              wametumia mtazamo wa kidhanifu katika kufasili dhana za fani na maudhui.


                64                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   64
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   64                    23/06/2024   17:54
   70   71   72   73   74   75   76   77   78   79   80