Page 76 - Fasihi_Kisw_F5
P. 76

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Wataalamu hawa huitazama fani na maudhui kama chungwa na ganda lake au
              kikombe na chai.

              Zifutazo ni hoja za mtazamo wa kidhanifu:
          FOR ONLINE READING ONLY
              (a)  Fani na maudhui  ni kama chungwa  na ganda  lake: Mtazamo huu
                   unayaona maudhui kama nyama ya ndani ya chungwa na fani ni ganda
                   lake la nje ambalo huifunika nyama hiyo. Mtu anapotaka kula chungwa

                   huliondoa ganda lake na kulitupa, kwani lengo huwa ni kuipata nyama ya
                   ndani. Kwa mtazamo huu, fani na maudhui huweza kutenganishwa. Hivyo,
                   mtunzi anapotunga kazi yake huwa hana haja na fani kwani kusudi lake ni
                   maudhui ambayo hulengwa kwa hadhira husika. Maudhui lengwa huweza

                   kuifikia jamii hata kama hayajafumbatwa na fani. Hadhira inaposoma kazi
                   hiyo hutafuta maudhui na si fani iliyoifunika kazi hiyo.

              (b)  Fani  na maudhui kama kikombe na chai: Mtazamo  huu umejitokeza
                   katika  kazi za baadhi ya watalaamu  wa fasihi. Miongoni mwao ni
                   Nkwera (1978) ambaye  anashadidia  kuwa fani  na maudhui  vinaweza

                   kutenganishwa na kwamba kila kimoja kinajitegemea kama ilivyo kikombe
                   na chai. Kikombe hutumika kubeba chai ili mnywaji aweze kuinywa. Chai
                   ikinyweka kikombe huwa hakina kazi tena. Hapa kikombe kinawakilisha
                   fani na chai ni maudhui katika kazi za fasihi. Hii ina maana kuwa mtunzi

                   wa kazi ya fasihi hulenga kufikisha maudhui kwa jamii na fani huwa ni
                   kibebeo chake tu. Mtazamo huu unaona kuwa mtunzi anaweza kufikisha
                   maudhui kwa hadhira yake bila kutumia fani.

              Mtazamo wa kiyakinifu
              Mtazamo  wa kiyakinifu huitazama  fani na maudhui kama vipengele
              vinavyotegemeana na ambavyo haviwezi kutenganishwa. Hii ni kwa sababu fani
              na maudhui hutegemeana, huathiriana na kujengana. Mtazamo huu hulinganisha
              fani na maudhui kama pande mbili za sarafu. Ifuatayo ni hoja kuu ya mtazamo
              wa kiyakinifu:

              Fani na maudhui kama pande mbili za sarafu moja: Mtazamo huu unaungwa
              mkono na Senkoro (1982 na 2011) unafananisha fani na upande wa kwanza wa
              sarafu, ilhali maudhui ni upande wa pili. Hii ina maana kwamba pande mbili
              za sarafu ndizo huikamilisha  sarafu hiyo; hivyo, haziwezi  kutenganishwa.


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            65
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   65                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   65
   71   72   73   74   75   76   77   78   79   80   81