Page 72 - Fasihi_Kisw_F5
P. 72

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (b)  Kuburudisha jamii
              Mchango mwingine wa fasihi simulizi na andishi ni kuburudisha jamii. Katika
              kutimiza jukumu hili, fasihi hustarehesha, huliwaza na kutuliza mwili na akili ya
              hadhira. Kwa mfano, watu wanapotazama vichekesho na maigizo ya “Mizengwe”
          FOR ONLINE READING ONLY
              (katika ITV Tanzania) hufurahia vituko, kejeli na mizaha inayoigizwa.

              (c)  Kuutambulisha na kuendeleza utamaduni
              Fasihi simulizi na andishi husaidia kuutambulisha, kuutangaza na kuuendeleza
              utamaduni. Kwa mfano, kazi mbalimbali za fasihi simulizi na fasihi andishi ya
              Kiswahili huakisi vipengele mbalimbali vya utamaduni wa Mswahili. Mifano ya
              vipengele hivyo ni desturi, dini, mavazi, mila, vyakula, na namna ya kuhusiana.
              Vilevile, mchango mwingine ni kuchangia katika kutunza amali na kumbukumbu
              nyingine za jamii. Mifano ya amali hizo za kijamii ni mila, desturi, historia na
              sanaa. Tamthiliya za Kiswahili kama vile Kinjekitile (Hussein, 1969) na Ngoma
              ya Ng’wanamalundi (Mbogo, 1988) zimebeba vyema jukumu hili la kuhifadhi
              na kurithisha amali za jamii. Pia, zinafafanua masuala ya kijadi kama vile imani
              na uganga.


              (d)  Kuadibu na kunasihi jamii
              Mara nyingi, fasihi hutumika kama nyenzo ya kuasa na kuadibu kuhusu mambo
              mbalimbali yanayojitokeza katika jamii. Kwa mfano, tamthiliya ya Ngoswe Penzi
              Kitovu cha Uzembe (Semzaba, 1988) inawaadibu na kuwaasa watu kufanya kazi
              kwa nidhamu.  Kwa ufupi,  tamthiliya  hiyo  inatoa  funzo  kwamba  mtaka  yote
              kwa pupa, hukosa yote. Katika fasihi simulizi, nyimbo hutumika kukamilisha
              jukumu hili. Kwa mfano, baadhi ya nyimbo za bongo fleva zina wasihi watu
              kupambana na harakati za maisha kwa kutafuta fursa za kiuchumi, bila kujali
              umbali unaoweza kusababisha utengano wa kifamilia.


              (e)  Kukuza na kuhifadhi lugha
              Fasihi simulizi na andishi ina mchango mkubwa katika kuikuza lugha. Lugha
              haiwezi kudumaa kwa sababu inakuwa kwenye matumizi. Mwanafasihi hutumia
              maneno kuibua na kueleza dhana mbalimbali katika utunzi wa kazi zake. Uandishi
              na usimulizi wa kazi za fasihi huibua misemo mipya mara kwa mara; kwa njia hii
              lugha huweza kukua. Kwa mfano, katika riwaya ya Kusadikika (Robert, 1991)
              kuna uibuaji wa msamiati kama vile ‘ali ali’ (tukufu) ‘azali’ (asili au kiini) ‘kitali’
              (mapigano) na ‘mlizamu’ (chemchem).

              (f)  Kutia hamasa jamii
              Fasihi hutia hamasa kuhusiana na mambo mbalimbali yanayotendeka  katika
              jamii. Mathalani, riwaya ya Pepo ya Mabwege (Mwakyembe, 1980) inatia hamasa


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            61
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   61                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   61
   67   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77