Page 67 - Fasihi_Kisw_F5
P. 67

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                 7.   “Hadithi fupi ni utanzu usioeleweka” Jadili kauli hii kwa mifano.

                 8.   Jadili maendeleo ya riwaya ya Kiswahili baada ya Uhuru.

                 9.   Eleza mchango wa mapinduzi ya viwanda katika kuzuka na kukua kwa
          FOR ONLINE READING ONLY
                     riwaya.

                 10.  Kwa kutumia mifano thabiti, jadili kauli kuwa fasihi simulizi ni malighafi
                     ya fasihi andishi.


              Uhusiano baina ya fasihi simulizi na fasihi andishi
              Licha ya kutofautiana, aina za fasihi zina uhusiano wa mwingiliano. Kwa mfano,
              kazi za fasihi andishi zina vipengele vya kifasihi simulizi kama vile semi, nyimbo
              na mazungumzo au dayolojia, wahusika wasio wanadamu (kwa mfano wanyama,
              mazimwi, wadudu na vinginevyo) na mbinu za uwasilishaji (mianzo na miisho
              ya hadithi, mianzo na miisho ya tenzi na nyinginezo). Mbali na mwingiliano,
              aina hizi za fasihi hutofautiana, kama inavyooneshwa katika jedwali lifuatalo:


              Tofauti kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi

               Na. Kigezo         Fasihi simulizi             Fasihi andishi
               1.   Utunzi        Huweza kutungwa mapema  Hutungwa kwa
                                  na kukaririwa kabla ya      kipindi kirefu kabla ya
                                  uwasilishaji. Huweza pia    kuwasilishwa kwa hadhira.
                                  kutungwa papo hapo wakati
                                  wa utendaji.
               2.   Uwasilishaji Huwasilishwa kwa njia ya     Huwasilishwa kwa njia ya
                                  mdomo, ishara na vitendo.   maandishi.
                                  Uwasilishaji huo hutumia
                                  viambato kama vile maleba,
                                  miondoko na sauti.
               3.   Umri          Ni kongwe kwa sababu        Ilianza baada ya
                                  ilianza kabla ya ugunduzi   mwanadamu kugundua
                                  wa maandishi.               maandishi.
               4.   Umiliki       Tanzu nyingi za fasihi      Ni mali ya mtunzi na
                                  simulizi ni mali ya jamii   mdhamini wake.
                                  nzima.








                56                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   56                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   56
   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71   72