Page 64 - Fasihi_Kisw_F5
P. 64

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              msanii za kumfanya msomaji awatuhumu watu wasiohusika ndizo zinazojenga
              maswali akilini mwa msomaji.

              (ii)  Hutumia wahusika wa kimwendelezo
          FOR ONLINE READING ONLY
              Riwaya pendwa zina sifa ya kutumia wahusika walewale;  hivyo, huwa na
              uwezo wa kujiendeleza katika vitabu kadhaa. Karibu kila mwandishi maarufu
              wa riwaya pendwa ameandika vitabu zaidi ya kimoja. Sifa hiyo ya kuwatumia
              wahusika walewale hufanya kitabu kimoja katika mfuatano wa vitabu kadhaa
              vya mwandishi mmoja kionekane kama tukio linalojitegemea katika mfululizo
              wa matukio mengi. Mifano ya watunzi waliowatumia wahusika wa jinsi hii
              ni  Aristablus  Elvis  Musiba.  Huyu  amemtumia  mhusika  Willy  Gamba  katika
              riwaya zake. Pia, Muhammed Said Abdulla amemtumia mhusika Bwana Msa
              katika riwaya zake takribani zote. Mwandishi mwingine ni Ben Mtobwa ambaye
              amemtumia mhusika Joram Kiango katika baadhi ya riwaya zake.

              (iii)  Huwa na mhusika mkuu mkwezwa

              Mhusika wa riwaya pendwa mara nyingi hupewa sifa zisizo za kawaida kitabia
              na kiutendaji. Mhusika mkuu wa riwaya pendwa hukwezwa juu ya wahusika
              wengine; hivyo, anatawala na ana sifa ya ubabe. Wahusika hawa huwa na sifa
              ya kuwa kielelezo chenye ukamilifu, yaani kutokuwa na dosari. Mifano mizuri
              ya wahusika wa namna hii ni Bwana Msa, Willy Gamba na Joram Kiango. Mara
              kwa mara, mhusika mkuu ndiye mshindi hata akipitia katika taabu na mashaka
              ya aina gani, tunajua, hatimaye ataibuka kuwa mshindi katika mapambano yake.
              Wahusika hawa wakuu hutenda na kuendesha mambo yao kama miungu wadogo
              pasi na kukosea. Huwa hodari sana katika kutenda mambo yao. Mambo hayo
              ni kama vile kuchunguza, kufanya mapenzi, kuwindana, kupigana kwa silaha
              na  kwa mikono  mitupu.  Kwa hiyo,  ufundi  wa utendaji  unaojitokeza  humo
              huwa unaziteka nafsi za wasomaji na, wakati mwingine, kuwasahaulisha hata
              maudhui. Mfano mzuri ni mhusika mkuu wa riwaya ya Njama (Musiba, 1981).
              Msomaji anapoendelea kuisoma riwaya hii, anajikuta anamezwa na ufundi wa
              kupeleleza na kupambana unaooneshwa na Willy na wenzake kiasi cha kupoteza
              kiini cha simulizi yenyewe, ambacho kinahusu ukombozi wa nchi za Afrika. Hali
              hii inasababishwa na hali ya kukwezwa kwa wahusika wa riwaya, hususani Willy
              Gamba, katika tabia na matendo yao.

              (iv)  Hupendwa na watu wengi

              Riwaya hizi zina wasomaji na wapenzi wengi, hasa vijana. Hii ni kwa sababu
              wasanii wake wameupatia vizuri utunzi wa kisasa ambao umeletwa na utamaduni



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            53
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   53                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   53
   59   60   61   62   63   64   65   66   67   68   69