Page 62 - Fasihi_Kisw_F5
P. 62

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (k)  Riwaya za kimaadili
              Hizi ni riwaya zenye nia ya kufundisha maadili  fulani yahusuyo mwenendo
              mwema katika maisha. Ni riwaya zinazowapa watu maadili,  na mara nyingi,
              maadili hayo huwa ya kidini. Wahusika wakuu huwa na sifa na tabia nzuri bila
          FOR ONLINE READING ONLY
              udhaifu. Sifa hizo ni za kudumu; kama ni mwenendo mwema huwa mwema tangu
              mwanzo hadi mwisho wa hadithi. Mabadiliko yakitokea, huwa ya kimaadili na
              hutokea ghafla. Mifano ya riwaya za aina hii ni Adili na Nduguze (Robert, 1952)
              Kisa cha Mrina Asali na Wenzake Wawili (Mnyampala, 1961) na Mtu ni Utu
              (Mhina, 1971).

              (l)  Riwaya za kimapinduzi
              Hizi  ni riwaya  zinazojadili matatizo  yanayosababisha  migogoro  fulani  katika
              jamii kwa lengo la kuleta mabadiliko. Mabadiliko hayo huweza kuwa ya kisiasa,
              kiutamaduni au kiuchumi. Aghalabu, lengo la riwaya hizi ni kuuwezesha umma
              kushika hatamu kwa njia ya mapambano. Mifano ya aina hii ya riwaya ni Ubeberu
              Utashindwa (Kiimbila, 1971), Kasri ya Mwinyi Fuadi (Shafi, 1974), Kabwela
              (Saffari, 1976), Dunia Mti Mkavu (Mohamed, 1979) na Kuli (Shafi, 1979).


              (m)  Riwaya za kifalsafa
              Riwaya za kifalsafa ni zile zinazojadili masuala anuai kuhusu maisha. Aghalabu,
              masuala hayo ni yale yanayohitaji tafakuri ya kina. Hii inamaanisha kuwa riwaya
              hizi zinajadili kwa kina na kwa kufanya tafakuri makini kuhusu mambo ambayo
              hayaonekani kwa urahisi. Muundo wa riwaya hizi ni changamani. Riwaya hizi
              hujadili maswali kuhusu maana ya ukweli, maisha au kifo kama vile ukweli ni
              nini? Maisha ni nini? Kifo ni nini? Kuwapo na kutokuwapo ni nini? Mifano
              ya riwaya za kifalsafa ni  Mzingile, Kichwamaji  (Kezilahabi,  1974),  Dunia
              Uwanja wa Fujo (Kezilahabi, 1978), Mafuta (Mkangi, 1984), Kiza katika Nuru
              (Mohamed, 1988), Nagona (Kezilahabi, 1989), Ziraili na Zirani (Mkufya, 1999),
              na Babu Alipofufuka (Mohammed, 2001).


              (n)  Riwaya za vitisho
              Hii ni  riwaya  yenye  visa vya kutisha  na kusisimua.  Mara nyingi,  visa  hivyo
              huambatana na mambo ya ajabu au miujiza. Mambo hayo ni kama vile mauaji
              ya kishirikina, uchawi, uganga na vita. Mifano ya riwaya hii ni Mbojo Simba
              Mtu  (Kuboja, 1971),  Mirathi ya Hatari  (Mung’ong’o, 1977) na  Janga Sugu
              la Wazawa  (Ruhumbika, 2002). Kwa mfano riwaya ya  Mirathi ya Hatari,
              imeeleza visa na mikasa ya kisihiri katika jamii za Njombe. Msanii amemtumia
              Gusto ambaye anarithishwa mirathi ya hatari (uchawi) kutoka kwa baba yake,
              Kazembe. Mirathi hiyo inasababisha vifo visivyokuwa vya kawaida. Miongoni



                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            51
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   51                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   51
   57   58   59   60   61   62   63   64   65   66   67