Page 65 - Fasihi_Kisw_F5
P. 65

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              wa kigeni unaofuatwa kwa makini na vijana na baadhi ya watu wazima. Kwa
              hiyo, watu wanaposoma riwaya hizi, wanasisimka na kuburudika.

              (v)  Hutumia mandhari ya mijini
          FOR ONLINE READING ONLY
              Wasanii wa riwaya pendwa hutumia mandhari halisi au ya kubuni, hususan katika
              miji au majiji. Hali hii ndiyo inayoonesha upekee wa mandhari ya riwaya pendwa.
              Wasanii hutumia mandhari ya namna hii ili kukidhi malengo ya usukaji wa visa
              na maisha ya wahusika. Mandhari ya namna hii hubeba matukio kama vile ufujaji
              mkubwa wa fedha kwenye sehemu za starehe, kama vile baa, hoteli kubwa na
              fukwe za bahari. Kwa mfano, kwenye riwaya ya Salamu Toka Kuzimu (Mtobwa,
              1987), kuna ufujaji mkubwa wa fedha unaofanywa na mhusika Joram na mpenzi
              wake. Vilevile, mandhari ya mjini yanaoneshwa kupitia tukio kama la uchezaji
              wa kamari linalojitokeza kwenye riwaya ya Simu ya Kifo (Katalambula, 1965).
              Aidha, mandhari ya mjini au jijini yanathibitishwa na kuwapo kwa kampuni na
              mashirika makubwa. Kampuni hizi huajiri watu. Waandishi huumba wahusika
              wenye vyeo kwa kuhusianisha na kampuni na mashirika hayo. Mfano mzuri ni
              mhusika Kalulu katika riwaya ya Pesa Zako Zinanuka (Mtobwa 1984). Huyu ni
              kiongozi katika kampuni mojawapo ya kusambaza dawa za Oxton. Mzee Jacobo
              kwenye Simu ya Kifo (Katalambula, 1965) ni mfanyakazi katika shirika la reli.

              Mandhari ya mijini pia hudhihirika kupitia matumizi ya vyombo vya mawasiliano
              kufanikisha matukio ya ujambazi, ujasusi, uporaji na uhusiano wa kimapenzi.
              Mathalani,  katika  riwaya ya  Najisikia  Kuua Tena  (Mtobwa, 1985), mhusika
              Kwame anatega chombo cha kunasa mawasiliano ofisini kwa Kombora. Chombo
              hiki  kinamsaidia  kunasa  maongezi  yote  ya  mipango  ya  kuwasaka  wahalifu
              (Kwame na kundi  lake).  Kwa njia  hii,  Kwame na kundi lake  wanang’amua
              mikakati ya kukamatwa, hivyo, wanafanikiwa kuwakimbia askari.


              (vi)  Matumizi ya wanawake kama nyenzo ya mafanikio
              Kwa ujumla,  wahusika  wakuu wa kiume  wa riwaya  pendwa  husawiriwa
              wakifanikiwa  katika  mambo yao kupitia  mbinu ya kuwatumia  wanawake
              warembo.  Warembo  hao hutumiwa  kwa njia  za  mapenzi,  kuwa chambo  cha
              kufanyia uhalifu, au chambo cha kumnasia adui. Mapenzi, kwa upande wake,
              huonekana  kuwa jambo  muhimu  sana  katika  riwaya  pendwa.  Huonekana
              kwamba, upelelezi  au shughuli yoyote inayofanyika  haiwezi  kusisimua wala
              kufanikiwa bila mapenzi. Katika riwaya za Musiba, kwa mfano, mhusika Willy
              Gamba huwa na wasichana warembo ambao ndio wapenzi wake wanaomsaidia
              kufumbua mafumbo mazito na mitego mikubwa. Baadhi yao ni Zabibu kwenye




                54                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   54                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   54
   60   61   62   63   64   65   66   67   68   69   70